0
                 RPC RUVUMA MIHAYO MSIKHELA
Na Stephano Mango,Songea

JESHI la polisi mkoani Ruvuma linamsaka mtu mmoja aliejulikana kwa jina Methid Ndomba mkazi wa kijiji cha Liwale wilayani Mbinga kwa tuhuma ya kumuua kwa kumkakata na kitu chenye ncha kali sehemu za kichwani John Mapunda(35)mkazi wa kijiji hicho na kuutekeleza mwili wa Mapunda katika kati ya bara bara ya kijijini hapo.


Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo lmetokea Agosti 3 mwaka huu majira ya saa 12 jioni katika kijiji hicho cha Liwale ambako inadaiwa mwili wa marehemu Ndomba ulikutwa kati kati ya bara bara ukiwa na majeraha makubwa huku damu zikiwa zimetapakaa kwenye eneo hilo.


Kamanda Msikhela alifafanua kuwa chanzo cha tukio hilo ulikuwa ni wivu wa mapenzi ambapo baada ya mwanamke mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa aliyedaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wawili hali iliyosababisha kuqepo kwa ugomvi mkubwa kati ya wanaume hao uliopelekea kuwepo na vitisho ambapo Ndomba inadaiwa kuwa aliwahi kumuonya marehemu Mapunda kwa kumtishia kuwa endapo ataendelea kuwa na mahusiano na huyon mwanamke atamfanyia kitu kibaya lakini Ndomba hakuweza kumsikiliza na aliendelea na mahusiano na huyo mwanamke.


Alieleza zaidi kuwa baada ya kuona kuwa Mapunda amepuuza onyo hilo alilopewa ndipo mtuhumiwa Ndomba alipoamua kumvizia Mapunda na kuanza kumpiga kwa kumkakata na kitu chenye kali kisha kumtemlekeza na kutokomea kusikojulikana.


Aidha Kamanda Msikhela alisema kufuatia tukio hilo jeshi la polisi mkoani Ruvuma linamsaka mtuhumiwa huyo na pindi atakapokamatwa atafikishwa kwenye vyombo vya kisheria kujibu shitaka linamlomkabili.


Mwisho.

Chapisha Maoni

 
Top