0

Na Gideon Mwakanosya-Songea
 
SIKU MOJA kabla ya kuanza mtihani wa darasa la saba mwanafunzi wa shule ya msingi Safina wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma Benedict Ndunguru (14) amekufa papo hapo baada ya kugongwa na gari  mda mfupi akitokea shuleni.
 
Akizungumza na Mtandao huu jana mchana ofisini kwake kaimu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Revocatus Malimi alisema kuwa tukio hilo lilitokea septemba 8 mwaka huu majira ya saa 12 jioni huko katika kijiji cha Buruma wilayani Mbinga.
 
alifafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio  huko katika kijiji cha Buruma kwenye barabara inayotoka mbinga mjini kwenda Mbambabay wilayani nyasa gari lenye namba za usajiri DFPA 1128 aina ya Toyota Hilux inayomilikiwa na shirika la umeme Tanzania (TANESCO) Wilayani Mbinga ambalo lilikuwa linaendeshwa na Samwel Mwambipile (33) mkazi wa Mbinga mjini likiwa kwenye mwendo mkali  lilimgonga mtembea kwa miguu Ndunguru na kumsababishia kifo papo hapo.
 
alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi  wa gari hilo ambapo dereva alishindwa kuhumudu usukani na kusababisha kutokea ajali hiyo na jeshi la polisi tayari linamshikilia dereva wa gari hiyo huku likiendelea kufanya uchuguzi wa tukio hilo la ajali na baadaye ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalomkabili.
 
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top