0



 MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU

NA STEPHANO MANGO,SONGEA
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili kuanzia kesho mkoani Ruvuma ikiwemo kukagua na kuzindua mradi mkubwa wa uranium katika mto Mkuju Wilaya ya Namtumbo na alahasiri atafanya mkutano wa kuwaaga wananchi wa mkoa kwenye uwanja wa majimaji

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alisema kuwa Rais Kikwete atawasili Mkoani Ruvuma leo asubuhi kwa ndege na atapokelewa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa Dini na wananchi kwenye uwanja wa ndege wa Songea

Mwambungu alisema kuwa mara baada ya Rais Kikwete kuwasili na kusaini kitabu cha wageni ataelekea wilayani Namtumbo kwa ajiri ya kutimiza wajibu wake wa kiserikali wa kukagua na kuzindua mradi mkubwa wa uchimbaji wa Uraniam katika mto mkuju na kasha atarudi mjini Songea na kufanya mkutano mkubwa wa hadhara wa kuwaaga wananchi baada ya utumishi wake wa miaka 10

Alisema kuwa siku ya jumatano ambayo ni Octoba 21 Rais Kikwete atarejea Jijini Dar Es Salaam kuendelea na majukumu yake mengine ya kiserikali

“Nawaomba wananchi waliopo katika maeneo mbalimbali mkoani humo wajitokeze kwa wingi kumpokea na kumsikiliza Rais Kikwete kwenye uwanja wa Majimaji ambaye kimsingi ameutendea mambo mengi mazuri Taifa na Mkoa wa Ruvuma”Alisema Mwambungu

Alisema kuwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wamepata bahati kubwa sana ya kuagwa na Rais Kikwete ikiwa ni siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Octoba 25 mwaka huu ambapo wananchi watatumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top