0



NA, STEPHANO MANGO, SONGEA

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imetoa jumla ya Shilingi milioni 259.5 kwa ajiri ya utekelezaji wa Ujenzi wa Maabara katika shule Sekondari 23 za Sekondari zilizopo katika Halmashauri hiyo

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani lililofanyika juzi kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo Mkurugenzi wa Wilaya ya Songea Sigsibert Valentine alisema kuwa Halmashauri inaendelea kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete la ujenzi wa Maabara tatu kwenye kila shule ya  Sekondari wilayani humo

Valentine alisema kuwa hadi kufikia desemba mwaka 2014 halmashauri yake ilikwishatoa fedha na vifaa vya viwandani vyenye thamani ya shilingi milioni 259,582,239 kwa ajiri ya ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara

Alisema kuwa fedha hizo zimetumika kuwalipa mafundi na ununuzi wa vifaa vya viwanda ambavyo vimekamilisha ujenzi huo na kwamba kilichobaki kwa asilimia kubwa ni ujenzi wa miundombinu ya ma maabara na chumba cha maandalizi(Preparation room), kufunga mitungi ya gesi na kupaka rangi majengo hayo

Alifafanua kuwa Sekondari zingine zipo kwenye hatua ya mwiso wa ujenzi kwani zinamalizia ujenzi wa maabara hizo kwa kufunga lenta na kupaua na tayari kwenye akaunti za shule zimeshaingizwa fedha kwa ajiri ya kukamilisha ujenzi huo haraka iwezekanavyo

Alizitaja Sekondari hizo ambazo zinajengwa maabara tatu kwa kila sekondari kuwa ni Sekondari ya Nguruma, Maposeni,Nalima, MagingoLipupuma na Gumbiro zikiwa ni sekondari za kata wilayani humo                                                                                                                                                                                                           

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Muhukuru Rajabu Mtiula aliwataka Wakuu wa Idara waliopewa majukumu ya kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa hatua zote wasimamie vyema rasilimali zote zinazotolewa na Halmashauri

Mtiula alisema kuwa kila muu wa Idara anapaswa kutumia nguvu zake zote kuhakikisha ujenzi huo unafanikiwa kwani licha ya kuwa ni agizo la Rais Jakaya Kikwete lakini ni muhimu sana kwani ni ukombozi mkubwa kwa wanafunzi ambao kwa muda mrefu hawakuwa na maabara za kujifunzia masomo yao ya Sayansi
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top