0

KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUVUMA MIHAYO MSIKHELA

NA STEPHANO MANGO,SONGEA

MWALIMU wa Shule ya Msingi Kaijere iliyopo katika kijiji cha Namabengo wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma Shaib Niali(30) amekutwa amekufa huku akinin’ginia kwenye kenchi ya nyumba yake baada ya kujinyonga kwa kutumia kanga

Habari zilizopatikana jana mjini Songea ambazo zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela zilisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa nane usiku kwenye chumba chake alichokuwa analala

Msikhela alifafanua zaidi kuwa inadaiwa Niali saa moja usiku kabla hajajinyonga alimpigia simu dada yake Asia Niali Mkazi wa majengo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kumjulisha kuwa anaumwa sana na alimuomba aende haraka kijijini Namabengo akamuone na kisha ampeleke nyumbani kwa mama yake mzazi alioko katika kijiji cha Lusewa

Alifafanua kuwa inadaiwa Niali kwa muda mrefu alikuwa ana ugomvi mkubwa na mke wake ambaye baadaye walilazimika kutengana lakini Niali alionekana kutokubali kukaa na watoto jambo ambalo lilikuwa linaleta ugomvi wa mara kwa mara

Alisema kuwa Niali wakati anampigia simu dada yake ya kumtaka afike kumuona Namabengo tayari alikuwa ameandaa kanga ya kujinyongea na panga kwa lengo la kutaka kwenda kumcharanga mke wake ambaye anaishi mbali kidogo na nyumba yake

Alieleza zaidi kuwa muda mfupi baada ya dada yake kupigiwa simu na kaka yake, Asia  aliwasiliana na majirani wanaoishi na Niali usiku huo ili kujua kinachomsibu kaka yake, ndipo majirani wakaenda nyumbani kwa Niali na kumkuta akiwa amejinyonga na kwamba majirani hao waliwasiliana na Viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Namabengo na taarifa ikapelekwa kwenye kituo cha Polisi cha Wilaya ya Namtumbo

Msikhela alieleza kuwa Askari Polisi walipopata taarifa ya Tukio hilowalienda haraka kwenye eneo la tukio wakiwa wameongozana na Daktari ambaye ndiye ayethibitisha kuwa Mwalimu Niali amekufa kwa kujinyonga kwa kanga na kwamba upeleleza wa tukio hilo unaendelea
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top