0
HILDA AKIWA AMEJERUHIWA na wananchi wanaomwita mchawi
mauruci akigugumia maumivu baada ya kichapo


WAWILI WAJERUHIWA KWA TUHUMA ZA USHIRIKINA PERAMIHO

NA STEPHANO MANGO,SONGEA
KATIKA hali isiyokuwa ya Kawaida watu wawili wakazi wa Kijiji cha Muunganozomba kata ya Kilagano Peramiho wamechezea kichapo kikali kwa kutumia malungu,panga na fimbo na kuwasababishia majeraa makali kwenye sehemu mbalimbali za miili yao na kulazwa katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Songea

Uchunguzi  uliofanya na Gazeti hili umebaini kuwa watu hao wamecharazwa bakora, panga na virungu kwa madai kuwa wamemficha mtoto aliyefahamika kwa jina la Adam Mselewa(4) katika mazingira ya kutatanisha yaani kiushirikina katika kijiji hicho

Tukio hilo lilitokea juzi kijijini hapo ambapo kundi la watu ambao wanasadikiwa kuwa ni wana ukoo liliwashambulia Hilda Johnfan Pili(79) ambaye amejeruhiwa vibaya kichani, mguu wa kulia na jicho la kushoto na Maurusi Zenda( 46) aliyejeruhiwa vibaya kichwani na mkono wa kushoto kutokana na kipigo walichokipata

Gazeti hili lilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela ili aweze kunipa kinagaubaga wa tukio hilo la kinyama na kusikitisha kutokea katika eneo hilo na hatua zilizochukuliwa dhidi ya watuhumiwa wa tukio hilo

Akizungumza na gazeti hili Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihaya Msikhela alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba  watuhumiwa kumi wamekamatwa kutokana na tukio hilo  na aliwataja watu hao ambao wanadaiwa kushiriki  kuwa ni Ambros Mselewa(24) ambaye ni baba mzazi wa mtoto aliyepotea, Maria Zenda(45) Lameck Zenda(22) Pautas Komba(24) Fredy Mende(24)Gerord Ngonyani(27)Odilo Mwingira(21) Shadrack Ngonyani(22) Hilda Zenda(36) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Muunganozomba

Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya 1;00 asubuhi huko katika Kijiji cha Muunganozomba ambako watu wawili walinusurika kuuawa baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali walioamua kujichukulia sheria mkononi kwa madai ya kushoshwa na vitendo vyao vya kishirikina

Alifafanua zaidi kuwa Inadaiwa chanzo cha tukio hilo ni kupotea kwa mtoto Adam katika mazingira ya kutatanisha Kijijini hapo tangu Februari 3 mwaka huu ambako Baba mzazi wa mtoto huyo Ambros Mselewa akishirikiana na baadhi ya watu ambao walikuwa na hasira kali waliwavamia watu hao wawili na kuanza kuwashambulia kwa madai kuwa wamemficha mtoto Adamu kwa mazingira ya uchawi

Alisema kuwa  Polisi baada ya kupata taarifa ya tukio hilo wakiwa wameambatana na Kamanda wa Polisi Mkoa walifika kwenye eneo la tukio mara na kuwakuta watu hao wawili wamejeruhiwa vibaya na jitihada za kuwaokoa na kuwapeleka katika Hospital ya Mkoa wa Songea ili wapatiwe matibabu

Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Hilda Johnfan Pili(79) ambaye amejeruhiwa vibaya kichani, mguu wa kulia na jicho la kushoto na Maurusi Zenda( 46) aliyejeruhiwa vibaya kichwani na mkono wa kushoto kutokana na kipigo walichokipata

Alieleza zaidi kuwa kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wote kuacha mara moja tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake wanapokuwa na watuhumiwa wahakikishe wanawapeleka kwenye vyombo vya dola

Kwa upande wake Daktari Mfawidhi wa Hospital ya Mkoa wa Songea Benedicto Ngaiza alithibitisha kupokea majeruhi hao na kwamba wamelazwa katika Hospital hiyo kwa ajiri ya matibabu na mara hali zao zitakapoimarika wataruhusiwa kurudi majumbani mwao
MWISHO





Chapisha Maoni

 
Top