0


Rais Jakaya Kikwete akiwa na Lowassa kwenye moja ya mikutano ya kisiasa

NA,STEPHANO MANGO,SONGEA

JUMAPILI februari mosi Mwaka huu majira ya Saa tatu asubuhi nikiwa nimeambatana na waandishi wenzangu  wa habari kutoka vyombo mbalimbali tulikuwa kwenye maeneo ya uwanja wa ndege wa Songea Mjini kwa ajiri ya kuwapokea Viongozi Mbalimbali waandamizi wa chama na Serikali

Nikiwa uwanjani hapo na wenzangu nawaona watu wakiwa wamesimama makundi makundi wakiwa wanazungumza mambo kadha wa kadha huku wakipanga mikakati ya kuwapokea viongozi wao ambao walikuwa wanakuja kwa ajiri ya Maadhimisho ya miaka 38 ya Chama cha Mapinduzi ambayo Kitaifa yamefanyikia Mkoani Ruvuma Katika Uwanja wa Michezo wa Majimaji

Nikalisogelea kundi moja wapo ili kutaka kujua wanajadiliana nini Uwanjani hapo, kumbe yalikuwa ni mazungumzo ya kuwapokea viongozi wao lakini kubwa lilikuwa ni shauku ya kumuona Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa

Sikuchelewa kudadisi kwa mmoja wa Mshiriki wa Kundi lile ambaye alitambulika kwa haraka  kwa jina la Hamis kutoka Wilaya ya Namtumbo, nilipomuhoji kulikoni mbona wanashauku ya kutaka kumuona Mbunge wa Monduli kuliko viongozi wengine waandamizi wa chama na Serikali

Jamaa akanijibu kuwa Makundi yote haya unayoyaona hapa uwanjani tunashauku ya kumuona Rais ajaye na tunataka kumwambia asife moyo na changamoto ambazo anakutana nazo ndani ya chama kwa sasa kwani wao wanampenda na wanaimani naye

“Leo tunahamu sana ya kumshangilia Mpendwa wetu Lowassa kwani kwa muda mrefu ajaigusa ardhi ya Mkoa wa Ruvuma na kwamba Viongozi wengine ambao wanafika Leo sio wageni kwani ni mara kwa mara wanafika na hakuna wanachokifanya zaidi ya kumaliza fedha za wananchi kwa kigezo cha ziara huku maamuzi wanayoyatoa hayatekelezeki”alisema kijana yule

Kijana yule nilizungumza nae mambo mengi sana yenye busara na hekima kuhusiana na mchakato mzima wa kuwapata wagombea wenye kukubalika miongoni mwa jamii wa ngazi zote za uwakilishi kwa maana ya Udiwani, Ubunge na Urais mpaka ndege inashuka uwanjani ndipo tulipoachana kwa kupeana namba za simu ili muda mwingine tuwe tunasalimia na kujadiliana mambo muhimu nchini

Niliachana na Kijana yule na kuwafuata waandishi wenzangu ili tupate maelekezo ya watu wa Itifaki namna ya kuweza kupata matukio muhimu uwanjani hapo, mara ndege inashika ardhi ya Mkoa wa Ruvuma na inatafuta uelekeo wa egesho lake ili iweze kushusha abiria waliokuwamo ndani ya ndege hiyo

Wakati tunajipanga Kuangalia wanaoshuka ndani ya ndege hiyo tuliona watu wachache wakishuka na mwisho akashuka Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa huku akipunga mikono na kuwafanya watu waliokuwepo Uwanjani hapo kulipuka kwa shangwe na vigelegele hali iliyomfanya asalimiane na watu hao huku akitafakari na baadae msafara wake ukaelekea eneo la maadhimisho

Wanahabari tuliambatana naye tukiwa na viongozi wengine kuelekea katika uwanja wa Majimaji ili tuufikishe msafara wake na kurudi tena Uwanja wa ndege ili kuwapokea wageni wengine kwani hata Mgeni Rasmi wa Maadhimisho hayo ambaye ni Mwenyekiti wa Ccm na Rais Jakaya Kikwete alikuwa bado hajawasili

Wakati Tunaingia Uwanja wa Majimaji Mshereheshaji wa Shughuli hiyo ya Maadhimisho kwa jina maarufu ni MC ambaye alitambulika kwa Jina la Nyakia Ally ambaye ni Kiongozi wa Chama cha Mapinduzi alipoutambulisha Msafara wa Lowassa na kusababisha pia watu waliokuwepo uwanjani hapo washangilie mpaka Lowassa anashuka ndani ya gari.

Mara baada ya Kushuka ndani ya gari Lowassa alilazimika kuwapungia mikono kushoto na kulia watu waliopo Uwanjani hapo huku akiachia tabasamu na kupunga mkono kushoto na kulia na kushangiliwa kwa vigelegele na vifijo na kuelekea Jukwaani kwa kupanda ngazi kwa kukimbia kwa ajili ya kupata nafasi yake ya kukaa ili aweze kuwapokea Viongozi wake wa Chama na Serikali

Sie Tulirudi tena Uwanja wa Ndege kumpokea Rais Na wageni wengine walioambatana nae na kurejea tena uwanjani hapo tukiambatana na Viongozi wengine waandamizi wa chama na Serikali wa Mikoa na Taifa na kwenda nao Ikulu ndogo ya Songea kabla ya kuingia kwenye uwanja wa Maadhimisho ya miaka 38 ya Chama hicho.

Mara baada ya Rais Kuingia uwanjani hapo ratiba iliendelea kama ilivyopangwa na mamlaka zinazohusika lakini cha kushangaza sio Katibu wa Itikadi, Siasa Na Uenezi Nape Nnauye, Katibu Mkuu wa Ccm Abrahamu Kinana, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadhimisho Dkt Emmanuel Nchimbi na Mwenyeki wa Ccm Rais Kikwete ambaye alithubutu kutambulisha Makada wa ngazi ya Kitaifa waliokuwepo ndani ya Uwanja huo

Makada hao waliokuwepo kwenye Maadhimisho hayo ni wale ambao wametangaza nia ya kuwania kiti cha urais mwaka huu ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa KImataifa Benard Membe, Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Mwigulu Nchemba, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Stephen Wassira waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

Kitendo cha kushindwa kutambulishwa Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu pekee aliyehudhulia  maadhimisho hayo kimetafsiriwa na wengi kuwa ni mkakati maalumu ulioandaliwa na maafisa usalama baada ya kuona upepo wa shangwe alipokuwa anashuka uwanja wa ndege na alipoingia ndani ya uwanja wa maadhimisho

Lowassa alipoingia Uwanjani hapo alikaa safu ya viti vya nyuma kabisa akifuatilia kwa umakini hotuba mbalimbali za Viongozi Ikiwemo hotuba ya Rais na mara baada ya Rais Kumaliza Hotuba yake na Mshereheshaji kumuinua mwanamuzi Diamond ili aweze kuburudisha wananchi waliohudhulia maadhimisho hayo

Watu wakiwa wanaendelea kumshangilia mwanamuziki huyo Lowassa alishuka jukwaani akatokea geti dogo lililopo chini ya jukwaa na kuondoka eneo hilo kabla Rais ajamaliza shughuli za maadhimisho hayo ikiwemo kukabidhi kadi kwa wanachama wapya wa Ccm, kukabidhi hundi ya Malipo ya Epz kwa Meya wa Manispaa kwa ajiri ya wananchi wa Kata ya Mwenge Mshindo

Kitendo cha wananchi kumshangilia Lowassa na Viongozi kushindwa kumtambusha kimenifanya nifikirie upya na kwa umakini na niandike makala haya ili wadau waweze kufanya tathimini katika mwenendo mzima wa mchakato wa kisiasa nchini na hasa katika wakati huu mgumu wa kupata Serikali ya awamu ya Tano

Rafiki yangu mmoja ambaye anafanya kazi Idara ya Usalama ya Taifa Mkoa wa Ruvuma nilipozungumza naye aliniambia kuwa Kitendo cha Lowassa kushangiliwa vile kinaonyesha namna alivyokuwa na ushawishi mkubwa miongoni mwa makundi ya  rika yote na makundi hayo yanamtaka Lowassa awe Rais wao ajaye na ndio maana hakutambulishwa kwani angetambulishwa uwanja mzima ungeripuka kwa shangwe na nchi nzima ingejua kwa sababu Redio na Televisheni zilikuwa zinarusha matangazo hayo hali ambayo ingeonekana kabisa kuwa chama kinampigia kampeni

Kitendo cha Lowassa kuondoka Uwanjani hapo kabla ya Rais na Viongozi wengine kutoka kwa kutumia mlango wa dharura kulinusuru kuharibu maadhimisho hayo kwani Makundi mbalimbali yalikuwa yanajipanga kumshangilia na kumshika mkoni ili iwe faraja yao katika kinyan’ganyiro cha Urais mwaka huu

Kutokana na hali hiyo ni lazima tuanze upya kwa kutafakari shangwe zile za Lowassa zinaleta picha gani kwa Taifa na jamii kubwa kuhusu muelekeo wake wa Kugombe Urais kama tunataka kufikia malengo yetu kama Taifa kwani kuanza upya huko kutaleta picha katika miaka 10 ijayo

Bila Kificho Lowassa ana kila aina ya sifa ya kuwa Rais wa Serikali ya awamu ya Tano kwani mara kadhaa ameonekanakukubalika kwenye makundi mbalimbali ya kijamii, kuelezea namna ya utatuzi wa changamoto mbalimbali za kitaifa

Watanzania tunayo njia ya kuelekea kwenye maendeleo ya kweli na njia hiyo ni Lowassa hivyo tunawajibika kuanza kufikiri na kujiandaa ili tuwe na uhakika wa ujenzi mpya wa Taifa letu litakalokuwa na sura tofauti kiuchumi,kijamii na kisiasa hapo kesho kwasababu kesho inategemea leo imeiandaaje kesho

Tufanye kitu cha maana leo ili kiweze kuleta usalama na ustawi kwa maaendeleo ya Taifa letu kesho na hapa cha muhimu tunachopaswa kujua ni kitu gani cha kufanywa kwa uhakika bila kubahatisha ili kuweza kuleta matokeo chanya 

Lowassa ameanza kazi kubwa na inahitaji gharama na itakayochukua muda wa miezi nane hivyo watanzania ni lazima tuthubutu kuanza nae safari mpya ya ukombozi wa Taifa letu ambalo kwa sasa linakabiliwa na changamoto nyingi sana

Ni lazima tuanze leo kwani tukiacha hadi kesho huenda tukachelewa katika mapambano hayo, tusikubali matokeo mengine bali ni ushindi wa jumla kwa jumla kama Taifa kwani wanashinda wale ambao wanaamini na wamejiandaa kushinda

Tukichukua hatua hatua ya kwanza leo na kuendelea kuchukua hatua ni dhahiri tutafika tunakolenga kufika katika kujenga taifa lenye sura mpya, lenye tija kwa kizazi hiki na kizazi kijacho hivyo tuchukue hatua sasa kujenga Taifa moja lenye nia moja na mstakabali mmoja

Tushirikiane pamoja kuipa nchi yetu nguvu mpya, dira mpya na mwelekeo mpya kitendo cha Lowassa kutangaza nia ya Kugombea Urais kimetusajiri rasmi katika mashindano mazuri ya kujenga taifa letu na katika hilo kushinda ni lazima kwani sharti muhimu la mashindano yoyote duniani ni ushindi

Ni muhimu watanzania tukamtafakari mpya Lowassa kwani ndie kiongozi pekee ambaye anaweza kuzikabili na kuzishughulikia changamoto za maendeleo kwa ujasiri na mkazo kutoka ndani yake na kuliunganisha taifa hili likawa lenye umoja na mshikamano

Kufikiri upya kutatupa mwanga mzuri wa kushikamana na Lowassa katika harakati zake za kuwania Urais kwani rekodi zake za utendaji ziko wazi na hiyo ndio nguzo yake kuu kwani ajasimama bila nguzo hivyo nguzo ni yale ya nyuma

Watanzania tukiamua tunafanikiwa kuitunza vyema tunu hiyo muhimu katika taifa letu kwani tunahitaji kuvuka salama katika uchaguzi wa mwaka huu hivyo bila kumpata kiongozi mwenye maamuzi magumu katika utendaji Taifa litayumba na kukosa muelekeo

Tunahitaji Kiongozi mwenye sifa kama za Lowassa kwani atakuwa mvumilivu siku zote bila kuchoka wala kukata tamaa mpaka malengo yatimie kwa manufaa ya waliomchagua kwani anatambua raha kupata ushindi katika mazingira magumu

Naamini kwamba tutafika pale kwenye kilele cha mafanikio kama tutafuata niliyoyasema kwa kuamua,kudhamiria na kutenda yaliyo chanya wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi ambao utaifanya nchi iweze kujengeka upya kisera na kiutendaji

Hakika Lowassa ni Kiongozi bora anayejari utawala, utu wa watu, haki zao, maslahi yao na usawa kati yao na asiyewatenga watu kwa matabaka wala kutengeneza madaraja katika jamii anayoiongoza na ndio maana katika uongozi wake katika serikali aliweza kusimamia vyema yale ambayo aliona yana maslahi makubwa kwa nchi bila kuteteleka na mafanikio yake tunayaona leo

Lazima tujenge upya tafakari zetu mwaka huu tukiongozwa na dhamira njema na kuziweka pembeni fitina, chuki, matusi na vurugu kwa viongozi wetu ambao tunaamini kuwa viongozi wazuri wanatoka kwa mungu hivyo ni lazima tutangulize maslahi mapana ya nchi yetu

Mwandishi wa Makala haya
Anapatikana kwa 0715-335051
Baruapepe;stephano12mango@yahoo.com

Chapisha Maoni

 
Top