MBUNGE WA PERAMIHO JENISTA MHAGAMA AKISISITIZA JAMBO
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
MBUNGE wa jimbo la Peramiho ambaye pia ni Waziri wa nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Uratibu wa Bunge ,Jenista Mhagama amewataka viongozi wa
Jumuiya za Wazazi,Vijana na
Jumuiya ya Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kutoka chama cha Mapinduzi(Ccm) kuhakikisha wanafanya kazi ya kuwahamasisha
wananchi kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na kuipigia
kura katiba pendekezwa ili kutoa fursa ya upigaji kura kwa wananchi wengi
katika kipindi cha uchaguzi mkuu ujao.
Wito huo umetolewa jana wakati wa hafla fupi ya kumpongeza Jenista Mhagama kupata nafasi mpya ya kuwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Parokia ya Bombambili Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi wote wa
jumuiya za chama hicho.
Wito huo umetolewa jana wakati wa hafla fupi ya kumpongeza Jenista Mhagama kupata nafasi mpya ya kuwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Parokia ya Bombambili Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na viongozi wote wa
jumuiya za chama hicho.
Alisema kuwa pamoja na mambo yote ya maendeleo yanayofanywa
na serikali inayongozwa na Ccm kazi iliyobaki katika kipindi hiki cha kuelekea
kwenye uchaguzi mkuu ni kuhakikisha wananchi wanajiandikisha kwenye daftari la
kupigia kura pamoja na kuipigia kura katiba pendekezi.
Jenista alieleza
zaidi kuwa kama viongozi wa jumuiya za chama hicho watasimama kidete kuhamasisha
kwa wingi wananchi kwenda kujiandikisha kwenye daftari hilo ,itatoa fursa kubwa kwa
wapigakura kushiriki kazi hiyo na hatimaye kukifanya chama hicho kuendelea
kushika dola .
“Ili chama chetu
kiendelee kushika dola ni lazima viongozi wa chama toka kwenye jumuiya zenu
kuinuka kwenda kufanya kazi ya kuhamasisha wananchi waende kujiandikisha kwenye
daftari la kudumu la kupigia kura na si
vinginevyo kwani vitambulisho vya kupigia kura vya zamani havitatumika na msidanganywe na wanasiasa wa
maji taka‘’alisema Waziri Jenista.
Aidha Waziri huyo licha ya kutoa maagizo hayo
aligawa Baiskeri 19 zenye thamani ya shilingi milioni 2.2 kwa jumuiya ya wazazi
ikiwa ni mwendelezo wa ahadi zake ambapo
tayari alishagawa baiskeli hizo kwa jumuiya zingine za vijana na UWT kwa
kila kata za jimbo lake .
Kwa upande wake katibu wa CCM wilaya ya Songea vijijini
Rajabu Uhonde akizungumza kwenye hafla hiyo kabla ya mgeni rasmi Jenista Mhagama kuzungumza na wanajumuiya hao alisema
kuwa chama chake kimejipanga vizuri kuhakikisha maagizo yote yaliyotolewa
toka ngazi ya taifa yanafanyiwa kazi kwa utekelezaji na aliwaonya wale wote
ambao wameonesha nia ya kutaka kugombea nafasi mbalimbali za uongozi
kwenye uchaguzi mkuu ujao wasubiri mpaka
muda utakapo fika vinginevyo watachukuliwa hatua za kinidhamu ndani ya chama.
Nao viongozi wa jumuiya hizo huku wakimshangilia Mbunge
huyo walisema kuwa wao hawafikirii kuchagua mtu mwingine kwa kuwa aliopo anatosha
kwa madai kuwa kawaletea maendeleo mbalimbali katika jimbo laozikiwemo barabara ambazo zilikuwa hazipitiki katika
vipindi vya nyuma ,elimu toka shule za sekondari 3 hadi kufikia 28,zahanati
pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa
kwa shule za msingi na kuongeza idadi ya walimu 349 waliopo sasa.
MWISHO.
MWISHO.
Chapisha Maoni