MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA SONGEA CHARLES MHAGAMA
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma
wamepitisha bajeti ya sh. 41,886,830,984 kutoka kwenye vyanzo vyake mbalimbali
vya mapato katika kipindi cha mwaka 2015 /2016.
Akisoma bajeti hiyo kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika
janakwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ya manispaa ,Mchumi wa
manispaa hiyo, Raphael Tumain Kimary alisema kuwa mchanganuo wake unatokana na
vyanzo vya mampato vya ndani vya halmashauri hiyo kiasi cha sh3,259,613,000.
Alisema kuwa mishahara ni sh.
24,710,969,400, matumizi mengine toka serikali kuu sh.2,296,844,000 ambapo
ruzuku ya miradi mbalimbali yamaendeleo sh.11,619,404,584 na vyanzo vya ndani
vya halmashauri hiyo ni sh.3,259,613,000.
Kimary alifafanua zaidi
kuwa vipaombele vya halmashauri hiyo ni kukamilisha miradi viporo ya majengo
katika zahanati na vituo vya afya,ukarabati wa ofisi kuu ,kata na mitaa,ujenzi
wa vivuko vya madaraja,sekondari,shule za msingi,pamoja na ujenzi wa nyumba za walimu
Mchumi huyo alivitaa vipaumbele
vingine kuwa ni kuboresha mitandao ya barabara kwa kiwango cha lami kwenye kata
mpya ambazo zimeongezwa ili ziweze kupitika kwa urahisi hasa kwa
kata ambazo zipo mbali na makao makuu na manispaa hiyo na kuendelea kutekeleza
mpango wa serikali wa tekeleza sasa kwa matokeo makubwa katika sekta ya
kilimo,elimu ,maji pamoja na mapato.
Kwa upande wake meya wa manispaa hiyo Charles Mhagama mara tu baada ya madiwani wote kuridhia kupitisha bajeti hiyo aliwataka kuonesha mfano kuwa mstari wa mbele hasa katika mwaka huu ambao unaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa madiwani,wabunge na Rais katika kuwahamasisha wananchi kushiriki shuhuli mbalimbali za maendeleo ambazo zitaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa manispaa hiyo kusonga mbele na madiwani wote kurudi kwenye baraza hilo kwa mara nyingine.
Kwa upande wake meya wa manispaa hiyo Charles Mhagama mara tu baada ya madiwani wote kuridhia kupitisha bajeti hiyo aliwataka kuonesha mfano kuwa mstari wa mbele hasa katika mwaka huu ambao unaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa madiwani,wabunge na Rais katika kuwahamasisha wananchi kushiriki shuhuli mbalimbali za maendeleo ambazo zitaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa manispaa hiyo kusonga mbele na madiwani wote kurudi kwenye baraza hilo kwa mara nyingine.
Mhagama ambaye pia ni
diwani wa kata ya Matogoro alisema kuwa kwa hivi sasa ni vyema kila diwani akajitahidi
kumalizia viporo vya miradi mbalimbali vya maendeleo kwa wananchi
wake ili waweze kuwa na imani nae na kumchaguwa tena kuwa diwani kwa mara nyingine.
MWISHO.
wake ili waweze kuwa na imani nae na kumchaguwa tena kuwa diwani kwa mara nyingine.
MWISHO.
Chapisha Maoni