Na STEPHANO MANGO,Songea.
MGOMBEA
wa udiwani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM katika kata ya Msamala
Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Isaacki Lutengano amewaahidi mambo
makubwa wananchi wa kata hiyo kuwa endapo watampa ridhaa ya kuwa
mwakilishi wao kwenye baraza la madiwani la Manispaa hiyo kazi ya kwanza
kuimarisha miundo mbinu ya barabara pamoja na kulimaliza tatizo la
upatikanaji wa maji ya bomba.
Lutengano
aliyasema hayo jana kwenye ofisi ya afisa mtendaji wa kata ya Msamala
muda mfupi baada ya kurejesha fomu ya kuwania nafasi hiyo aliyokuwa
ameichukua siku tatu zilizopita baada ya kuibuka mshindi na kuteuliwa
ndani ya chama hicho.
Alisema
kuwa licha ya kata hiyo kuwa na eneo kubwa la mraba lakini kumekuwepo
na changamoto mbalimbali za mambo ya kijamii ikiwemo na suala la
ukosefu wa miundombinu ya uhakika kama barabara hasa za kupita kwenye
mitaa.
Alieleza zaidi kuwa tatizo la upatikanaji wa maji katika eneo la kata
hiyo ni kubwa hivyo endapo atachaguliwa kuwa diwani wa kata hiyo kwa
kushirikiana na watalaamu wa idara ya maji watahakikisha kuwa tatizo
hilo linapungua au kuisha kabisa.
Kwa upande wake Happnes Haule ambaye ni mgombea udiwani viti maalumu
kupitia chama hicho aliwaeleza waandishi wa habari kuwa wagombea wote wa
udiwani kwenye kata hiyo wamekuwa na mshikamano wa pamoja hivyo endapo
watachaguliwa watakuwa msaada mkubwa kwa wananchi ambao wamekuwa
wakikabiliwa na changamoto nyingi.
Naye afisa mtendaji wa kata ya Msamala Esta Kosa alisema kuwa kata
hiyo mpaka jana mchana wagombea wa tatu wamesharudisha fomu ambapo
aliwataja kuwa ni ,Isaacki Lutengano wa CCM,Issa Chamajaa wa Chadema na
Kudeka Haule wa ACT ,Wazalendo.
MWISHO.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni