Mgombea Urais DKT MAGUFURI akimnadi mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini kwa tiketi ya CCM Leonidas Gama
NA STEPHANO MANGO, SONGEA
ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa
wa Kilimanjaro ambaye kwa sasa anagombea Ubunge kupitia chama cha Mapinduzi
(CCM) Jimbo la Songea Mjini Leonidas Gama amewaomba wananchi wa songea waone
umuhimu wa kumpa kura mgombea urahisi kwa tiketi ya ccm Dr. John Pombe Magufuli
kwa kuwa ni mtendaji kazi mzuri na ni mwadirifu.
Gama ameyasema hayo juzi kwenye uwanja wa Majimaji ambako umati mkubwa wa wakazi wa maeneo mbalimbali ya manispaa ya
songea walihudhuria kwenye mkutano wa kampeni
wakati akijinadi mgombea Urais, Ubungea na madiwani wa chama hicho.
Alisema kuwa Dr.
Mgufuli ni tingatinga ambalo limekuwa likifanya kazi kwa muda wote kwa lengo la
kuleta manufaa makubwa kwa watanzania wote hivyo anastahili kwa kiasi kikubwa
kuwa Rais ya Jamhuru ya Muungano wa Tanzania na si vinginevyo.
Gama pia amewaomba
wakazi wa manispaa songea kuona umuhimu wa kumchagua ili awe mbunge wao kwa
kuwa anatambua fika matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi ambao wengi wao ni wakulima na
wafanyabiashara.
Alisema kuwa songea
inachangamoto nyingi zinazotakiwa zifanyiwe kazi na mwakilishi mzuri kwenye
bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania hivyo yeye ni greda lenye uwezo wa
kusawazisha changamoto zote zilizopo ambazo wagombea wengine.
Mapema mgombea urahisi
Dr. Magufuli ambaye kwa muda wote wanashangiliwa na umati mkubwa wa watu
waliofika kumsikiliza wakati akijinadi alisema kuwa mkusanyiko mkubwa
uliojitokeza songea mjini ni wanasiasa
wa vyama vyote hivyo endapo atapewa ridhaa ya kuwa Rais atakuwa ni kiongozi
mwenye kuwajali watanzania wote bila kujali itikadi ya vyama.
Dr. Magufuli alisema
kuwa endapo atapata ridhaa ya kuwa rais wa nchi serikali yake haitaweza kuruhusu
wakulima wakopwe mazao yao bali itahakikisha wakulima wanatafutiwa masoko ya
mazao yao ya uhakika na kwamba kiongozi yeyote atayekwenda tofauti na maagizo
yake atamuajibisha.
MWISHO
Chapisha Maoni