0
 
        KAMANDA WA POLISI RUVUMA MIHAYO MSIKHELA
 
NA STEPHANO MANGO.SONGEA
 
JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma Linamtafuta Edwin Mrope (39) mkazi wa Lizaboni manispaa ya songea kwa tuhuma za kumpiga mtoto wake kichwani wa umri wa mwaka 1 na kumsababishia kifo wakati walipokuwa anamshushia kipigo mke wake aliyekuwa amembeba mtoto huyo mgongoni aliyetambulika kwa jina la Wapekee Mrope (1).
 
Akizungumza na mtandao huu jana mchana ofisini kwake kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Mihayo msikhela alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 12 jioni huko katika eneo la Lizaboni manispaa ya songea.
 
Kamanda Msikhela alisema kuwa tukio hilo limetokea wakati Mrope alipokuwa anagombana na mke wake Lucy Lupogo ambaye inadaiwa alishushiwa kipigo sehemu mbalimbali za mwili huku akiwa amembeba mtoto wake mgongoni na kisha alimvuta mkono wa kulia na kumsababishia uvimbe mkubwa kwenye mkono huo.
 
Alifafanua zaidi kuwa inaadaiwa wakati Lupogo anapigwa na mume wake huku akiwa amembeba mtoto Wapekee ghafla mtoto huyo alipigwa kichwani na fimbo na kumsababishia maumivu makali jambo ambalo lilisababisha wamkimbize hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi ambako baada ya kupokelewa mda mfupi tu alifariki dunia
 
Alisema kuwa uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha ugomvi ni kwamba Mrope alikuwa anadaiwa fedha alizokuwa amekabidhiwa na mke wake ili akamunulie vifaa vya ndani vya nyumba yao jambo ambalo lilileta mzozo wakati aliposhindwa kurejesha fedha au vifaa alivyoagizwa akanunue.
 
Alieleza zaidi kuwa  uchunguzi huo umebaini kuwa  fedha hiyo mke wake aliyekuwa anamdai mume wake alikuwa ameipata baada ya kuuza ufuta lakini mrope fedha hiyo alikuwa tayari ameshaitumia kwa starehe zake na kwamba kwa sasa hivi polisi inaendelea kumsaka mtuhumiwa huyo ambaye inadaiwa amekimbia kwenda mpakani mwa msumbiji na Tanzania lakini jitihada zinafanywa za kuhakikisha kuwa a
nakamatwa.
 
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top