JENISTA MHAGAMA AKIPOKEA ILANI YA UCHAGUZI WA CCM YA 2015-2020 TOKA KWA MGOMBEA URAIS DKT JOHN MAGUFURI
NA STEPHANO MANGO, SONGEA
JIMBO la Peramiho linaundwa na kata 16 zenye tarafa mbili za
Ruvuma na Mhukuru ni miongoni mwa majimbo tisa ya uchaguzi yalipopo mkoani
Ruvuma ambayo yanaendelea na harakati za kampeni za kuomba kura kwa wananchi
wake ili kuunda Serikali ya Awamu ya tano
Jimbo hilo ndilo Jimbo pekee mkoani Ruvuma ambalo lilikuwa linawakilishwa
na Mbunge mwanamke kupitia chama cha Mapinduzi(CCM) ambaye pia ni Waziri wa
Sera ,Uratibu na Bunge Jenista Joakim Mhagama kwa kipindi cha miaka 10 ya
Serikali ya awamu ya nne
Katika kipindi cha kura za maoni ndani ya Ccm Jenista
Mhagama ndiye mgombea pekee katika majimbo yote tisa yaliyopo mkoani Ruvuma
ambaye alipita bila kupingwa ndani ya chama chake kutokana na imani kubwa
kutoka kwa wanachama wenzake
Hicho ndicho kilichonifanya nifuatilie mikutano yake ya
Kampeni kwa wananchi ili niweze kujua anawaambia nini katika kipindi hicho cha
miaka 10 ambayo alikuwa anawawakilisha katika jimbo hilo muhimu kiuchumi na
kiutalii
Nimebahatika kuhudhuria mikutano yake mitano kwenye kata ya
Maposeni, Parangu, Peramiho,Kilagano na kata ya Litisha ambayo alikuwa
anaelezea utekelezaji wake wa ahadi na ilani ya chama chake kwa kipindi cha
miaka 10 iliyopita
“Nimejitahidi kutekeleza ilani ya ccm na ahadi zangu binafsi
kwa asilimia 95 katika sekta ya Elimu, afya, nishati ya umeme,maji,barabara na
ujenzi,Kilimo na ushirika,mifugo na uvuvi,ardhi na maliasili,biashara na
masoko,mawasiliano,uwekezaji, michezo na ajira”alisema Mhagama
Mhagama alisema kuwa jimbo hilo lenye kata 16 ikiwemo ya Matimira ,Kilagano ,Ndongosi, Mpandangindo,
Mbinga Mhalule, Mtyangimbole, Matumbi, Gumbiro, Nakahuga
Magagura,peramiho,Mpitimbi,Mhukuru,Maposeni,Parangu,Litisha kuna mambo mengi
sana yamefanyika kupitia sekta hizo kwa uchache nitayasema kwenye mikutano
yangu na mengine mtayasoma wenye kwenye kitabu changu cha utekelezaji wa ilani
kwa kipindi cha miaka 10 ya uwakilishi wangu
Nimefanikiwa kufika kwenye kila kijiji cha jimbo la peramiho
na kufanya mikutano mbalimbali ya kichama na kiserikali na kufanikiwa kuibua
miradi mingi na kuitekeleza katika sekta mbalimbali yenye tija na kuwafanya
wananchi waendelee kushikamana na serikali yao
Alisema miradi mbalimbali imetekelezwa na kuwafanya wananchi
waendelee kufurahia serikali yao kutokana na matumizi mazuri ya raslimali za
Taifa chini ya uongozi mahiri kutoka chama cha mapinduzi ukiongozwa na Rais
Jakaya Kikwete na watangulizi wake
Kwa kushirikiana na serikali ameweza kuhakikisha ujenzi wa
visima 16 vya maji katika kijiji cha liweta, masigira na likuyufusi,kujenga
miradi ya maji ya mtiririko katika vijiji vya lilondo,Maweso,Liula na maji ya
mtiririko wa Luyelela ambao unaunganisha vijiji 7 na kuwafanya wananchi wa
maeneo hayo kuondokana na adha ya maji
Kuna vijiji vichache bado vinakabiliwa na shida ya maji na
wataalamu wameshaanza kutafutia ufumbuzi changamoto hiyo na hasa kuvibaini
vyanzo muhimu vya maji na kuanza ujenzi wa miradi hiyo kwani kwa sasa huduma ya
maji katika jimbo hilo inapatikana kwa asilimia 85
Vikundi vya ujasiliamali vya wanawake, wazee na vijana
vimeundwa kwenye kila kata za jimbo hilo na kuwezeshwa fedha za mkopo na kupewa
miradi ya kufuga mbuzi, kuku, ng’ombe na nguruwe hali ambayo imesaidia
kupunguza kaya zilozo na umaskini
Katika sekta ya elimu kuanzia elimu ya awali, msingi na
Sekondari miundombinu imejengwa kwani kila kijiji kina shule ya msingi , kila
kata ina sekondari na maabara moja au mbili na kufanya watoto wengi kupata haki
hiyo ya elimu na kwamba kiwango cha ufauru kimeongezeka, wapo pia wanafunzi
ambao anawasomesha mbunge
Zipo bado changamoto katika sekta hiyo ikiwemo nyumba za
walimu, walimu wa sayansi ni wachache na baadhi ya sekondari hazina mabweni ya
kukidhi wanafunzi wote hivyo katika kipindi kijacho cha uongozi wangu
nitajitahidi kuyatatua
Sekta ya afya katika kipindi cha miaka 10 ya uongozi wangu
nimefanikiwa kuhakikisha kila kata ina zahanati na huduma bora ya afya
inatolewa kwa masaa 24 , ingawa zipo kata zina zahanati hadi mbili na kwamba
zahanati hizo zote nimeziwekea umeme wa jua, pia tuna vituo vitatu vya afya
pamoja na hospital moja hivyo wananchi wanapata huduma hiyo muhimu,
Alisema kuwa yapo mambo madogo madogo ambayo yanapaswa
yafanyiwe kazi katika siku za karibuni na hata ilani ya Ccm ya 2015-2020 yameainishwa vizuri ambayo yanalazimisha
Serikali ijayo kwa ushirikiano na Mbunge kuyafanya
Mtandao wa barabara katika kipindi cha miaka 10 nimejitahidi
kuongeza kwa kasi,ujenzi wa barabara toka wino hadi ifinga umeendelea
kuwakomboa wananchi wa eneo hilo, ujenzi wa vivuko , madaraja, na makalvet nao
umeongezeka, jambo ambalo nawajibika mara nitakapochaguliwa tena ni kujenga
barabara za kuunganisha vijiji vyote vya jimbo la peramiho na kuimarisha
barabara hizo ili zipitike muda wote na kuwafanya wananchi waendelee kufanya
shughuli zao za kujiletea maendeleo
Mhagama alisema kuwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa
maendeleo, serikali na Kanisa katoliki tumefanikiwa kusambaza umeme kwenye kata
chache lakini pia serikali kupitia umeme wa Vijijini(REA) imefanikisha
kufikisha umeme karibu kata zote na kwamba unaendelea kuunganishwa kwa wananchi
Lengo ni kuwafikiwa wananchi wote ambao wanataka nishati
hiyo kwa matumizi ya ujenzi wa viwanda vidogovidogo, matumizi ya majumbani na
matumizi mengine ya kiuchumi kwa vijana na kuwafanya washughulike na wajipatie
kipato
Sekta ya kilimo na ushirika tumejitahidi kutoa ruzuku ya
pembejeo za kilimo , zana za kilimo,na watu wamelima wengi sana na kufanya
uzalishaji wa mazao ya kilimo kuwa mkubwa, changamoto ambayo inatukabili kwa
sasa ni kuwa na viwanda vya kusindika mazao hayo, soko la uhakikia la ununuzi
wa mazao hayo
Jambo la kuwakopa na kuwalangua wakulima sasa mwisho kwani
ilani ya Chama imeitaka Serikali ijayo kusimamia kikamilifu na kuwajali
wakulima, hivyo nikichaguliwa naamini tutaibana serikali ili ihakikishe
inawajengea viwanda vya usindikaji mazao wakulima ili kupandisha thamani ya
mazao yao
Pia wananchi wameweza kujiunga kwenye vyama mbalimbali vya
kuweka na kukopo na kufanikiwa kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali,
kusomesha na kujenga vitega uchumi ambayo vinawaingizia vipato
Sekta ya mifugo na uvuvi nayo kwa kipindi cha uwakilishi
wangu niliiwekea vipaumbele sana kwani wapo wafugaji ambao walipewa mbuzi,
ng’ombe, kuku na nguruwe kwa mkopo na wapo wengine wamemaliza mikopo yao na
wanaendelea kunufaika na miradi hiyo mizuri ambayo inawaongezea lishe na kipato
Kwa upande wa uvuvi nimejitahidi kuwapatia wananchi wenye
mabwawa mbegu za samaki bora, na miradi ya uchimbaji wa mabwawa mapya
unaendelea na kwamba upimaji wa viwanja nao unaendelea kwa kasi na kuwafanya
wananchi wengi kumiliki mashamba na viwanja vya biashara na makazi
Sekta ya maliasili nimefanikiwa kuunda vikosi kazi vya
kulinda misitu, vyanzo vya maji, idadi ya wafugaji nyuki imeongezeka, mizinga ya nyuki nayo na uvunaji
wa asali umeongezeka,vitalu vya miche vimeongezeka, idadi ya misitu iliyotengwa
na kuhifadhiwa imeongezeka na hata uchomaji wa misitu ovyo umepungua
Upatikanaji wa simu kwa wakazi wa jimbo hilo umepanuka kwani
kwenye kata zote kuna mawasiliano na
upatikanaji wa televisheni, redio na magazeti nayo umerahisha wananchi kuelewa
mambo mengi ya kitaifa na kimataifa na kuwa fanya kuwa kijiji kimoja
Kwa upande wa utawala bora katika kata zote kuna ofisi ya
afisa mtendaji wa kata na katika vijiji vingi kuna ofisi ya mwenyekiti wa
kijiji jambo ambalo linarahisisha upatikanaji wa huduma za kiutawala kwa
wananchi
“Nimejitahidi katika kipindi cha mika 10 ya uwakilishi wangu
kuligawa jimbo la peramiho na kupatikana jimbo jipya la madaba na wilaya mpya
ya madaba jambo ambalo limepunguza kero za wananchi wa kata ya Wino,
Igawisenga,mkongotema ambao walikuwa wanasafiri umbali mrefu siku mbili hadi
tatu kufuata huduma songea” alisema Mhagama
Alisema wakati anaingia jimboni humo kwa mwaka 2005 hali ya
jimbo hilo ilikuwa mbaya sana katika sekta zote lakini nafarijika kwa kutimiza
ahadi zangu, na kitendo cha kuhamisha makao makuu ya halmashauri kutoka songea
mjini na kujenga makao makuu ya halmashauri kijiji cha Lundusi peramiho
kutaharakisha utatuzi wa changamoto ndogo zilizobaki ambazo kimsingi
zimeainishwa vizuri kwenye ilani
Leo nasimama kifua mbele nikiwa na furaha za kutekeleza
ilani ya Ccm ya mwaka 2005-2015, hivyo najitokeza mbele yenu tena kuomba kura
zenu ili niwe mbunge tena ili niweze kumalizia changamoto zilizobaki kwani kwa
ushirikiano mkubwa tutafanikiwa
Ni vema ikakumbukwa kwamba kufanya kazi pamoja ni umoja na
kudumu katika umoja ni maendeleo, hivyo tuunganishe vipaji vyetu viwe timu
moja ya mafanikio kwa maendeleo ya wanaperamiho kwa kuchagua viongozi bora wa
Ccm kwa nafasi ya Udiwani , urais na ubunge ifikapo octoba 25 mwaka huu
Wananchi
mnatakiwa kukipigia kura chama cha mapinduzi kwani kimeweza kuifanya
peramiho kuwa kioo cha maendeleo kitaifa na ing’ale
kimataifa kutokana na ushirikiano mlionionyesha kwa kipindi hiko chote
cha
miaka 10 ya uwakilishi wangu na ndio maana Rais Jakaya Kikwete kwa
kuwaheshimu
wananchi wa Jimbo la Peramiho aliweza kuniteua kuwa Naibu Waziri wa
Elimu na
Mafunzo na sasa kaniteua kuwa Waziri
Sera, Uratibu na Bungea , alisema Jenista
Mwandishi wa Makala haya
Anapatikana 0715-335051
MWISHO
Chapisha Maoni