KAMANDA WA POLISI RUVUMA MIHAYO MSIKHELA
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
JESHI
la Polisi mkoani Ruvuma linamsaka mganga wa kienyeji ambaye jina lake
limehifadhiwa mkazi wa eneo la Lilambo manispaa ya songea kwa tuhuma za
kumnywesha dawa Lucia Zimbili (65) mkazi wa kijiji cha Maposeni Peramiho ambaye
inadaiwa alikuwa analalamikiwa na ndugu zake kuwa amemroga Edward Soko
aliyefariki dunia siku chache kabla ya tukio hilo.
Habari
zilizopatikana jana ambazo zimezibitishwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma
Mihayo Msikhela zimesema kuwa tukio hilo limetokea Julai 12 mwaka huu majira ya
saa za usiku huko katika eneo la Lilambo nje kidogo ya manispaa ya Songea.
Kamanda
Msikhela alifanunua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio nyumbani kwa mganga
wa kienyeji ambaye jina lake limehifadhiwa mwanamke mmoja Lucia Zimbili
alifariki dunia baada ya kunywa dawa aliyokuwa amepewa na mganga wa kienyeji.
Alifafanua
zaidi kuwa Lucia alinyweshwa dawa hiyo na mganga wa kienyeji kwa lengo la
kutambua kama kweli alihusika au hakuhusika na kifo cha Edward aliyekuwa
amefariki Julaiu 7 mwaka huu huko katika kijiji cha maposeni nje kidogo ya mji
mdogo wa Peramiho.
Alieza
zaidi kuwa baada ya kufariki Soko inadaiwa ndugu wa ukoo walikaa na kisha
walimtuhumu Lucia kuwa ndiye aliyemroga na baadaye waliamua kwa pamoja kwenda
kwa mganga wa kienyeji kwa lengo la kubaini ukweli wa tuhuma hizo ambako walipofika
mganga wa kienyeji aliwapokea na alianza kuwasikiliza tatizo walilokuwa nalo.
Alisema
kuwa baadaye mganga huyo alianza kuwapa dawa ambayo aliwapa kwa masharti kuwa
dawa hiyo wanatakiwa kunywa kwamba kila mmoja atakayekunywa dawa hiyo madhara
yakimkuta ndio atakeyekuwa amehusika na kifo cha Edward ndipo kila mmoja alipoanza
kunyweshwa dawa ambayo mda si mrefu Lucia alianza kubadilika na kufariki dunia.
Hata
hivyo uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa mara tu baada ya kifo cha Soko
wanaukoo wote kwenye msiba chini ya uongozi wa Biatus Soko walikutana kwa
pamoja kwa lengo la kutafuta sababu za kufariki ndugu yao ambapo baada ya kikao
walimtuhumu Lucia kuwa ndiye aliyehusika kwa kifo cha ndugu yao.
Kamanda
Msikhela alifafanua zaidi kuwa kutokana Lucia kukataa kuhusika na tuhuma hizo
ndugu kwenye kikao cha familia hiyo waliamua kwa pamoja kwenda kumpeleka kwa
mganga kwa lengo la kuondoa ubishi uliojitokeza kati yao na Lucia.
Alisema
kuwa wanafamilia hao baada ya kifika kwa
mganga walipewa maelekezo yenye masherti ambayo baadaye baada ya kunyweshwa
dawa hiyo iliyomsababishia kifo Lucia na kwamba mganga huyo alipogundua Lucia
amepoteza maisha alikimbia na kutokomea kusiko julikana na polisi inaendelea
kumsaka.
MWISHO
Chapisha Maoni