0




Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Bw. Mtani akikabidhi baiskeli kwa Mgani Kazi wa kijiji cha Mtonya Bi. Zingua Moyo

Kaimu Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya ya Namtumbo Bw. Mtani (Mwenye Suti)akikabidhi baiskeli kwa Magani Kazi wa kijiji cha Mtonya Bi. Zingua Moyo,katika mwenye shati la mikono mirefu lenye langi ya bluu ni Afisa Ugani wa Taasisi ya ACTN Abiud Gamba

Bw. Saidi Chalamanda akiwa amepanda baiskeli aliyokabidhiwa kama Mgani kazi,wa kwanza kuliamwenye shati la mikono mirefu lenye langi ya bluu ni Afisa Ugani wa Taasisi ya ACTN Abiud Gamba

Kaimu Mkurugenzi Bi. Wenseria Swai akikabidhi moja ya baiskeli kwa wagani kazi 13 kwa niaba ya wenzao,wa kwanza kulia ni Afisa Ugani kutoka taasisi ya Mtandao wa Kilimo Hifadhi Afrika (ACTN) , Abiud Gamba 
NA STEPHANO MANGO,SONGEA

MAAFISA ugani wametakiwa kufanya kazi zao kikamilifu ili kuweza kuwasaidia wakulima kupata elimu bora ya kilimo ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao yao ya kiuchumi na kibiashara nchini



Wito huo umetolewa jana kwenye Viunga vya Ofisi ya Mkurugenzi Wilaya ya Songea na Afisa Ugani wa Taasisi ya African Conservation Tillage Network, ACTN  Abiud Gamba wakati wa tafrija fupi ya kukabidhi baiskeli kwa wakulima wa wilaya ya Namtumbo na Songea Vijijini



Gamba alisema kuwa maafisa ugani ni nguzo muhimu sana ya kukuza kilimo na kukifanya kiwe mkombozi mkubwa kwa wakulima na taifa kiujumla hivyo ni vyema maafisa hao wakaacha tabia ya kukaa maofisini na badala yake waende kwa wakulima na vikundi vyao kwenda kuwaelekeza kanuni bora za kilimo



Alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kilimo nchini ACTN kwa kushirikiana na washirika wake katika mradi wa Kuongeza Tija ya Uzalishaji nyanda za juu kusini mwa Tanzania (Integrated Bead Basket Project) wametoa baiskeli 25 kwa wakulima wa wilaya za Namtumbo na Songea vijijni ambao ni watoa huduma ya kuwawezesha wakulima wenzao maarufu kama wagani kazi katika elimu ya kilimo hifadhi



Alifafanua kuwa baiskeli hizo zitawasaidia kutafuta masoko, kuvitembeleavikundi vya wakulima, kutafuta pembejeo za kilimo na kutembeleana na kupeana elimu ya fedha katika vijiji vyao.



“Hii ni kuwawezesha wagani kazi hao waliojengewa uwezo na Taasisi hiyo ya ACTN kutoa elimu ya ugani na ushauri wa masuala ya kilimo katika jamii zao kwa kushirikiana na maafisa ugani wa vijiji husika” alisema Gamba



Alifafanua kuwa kwa Songea vijiji ambavyo vimenufaika na mradi huo ni Namatuhi, Mpitimbi, Litapwasi, Matimila, Gumbiro, Ngadinda, Mkongotema, Madaba na Lilondo na Kwa Namtumbo ni vijiji vya Kitanda, Naikesi, Luhimbalilo, Mtonya, Rwinga, Mandepwende, Namanguli, Litola na Mchomoro.



Alieleza kuwa baadhi ya majukumu yanayofanywa na Taasisi hiyo ya ACTN ni pamoja na kufanya tafiti za udongo ambo tayari sampuli za udongo zimeshachukuliwa kwenye vijiji hivyo kwa ajili ya utafiti kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti wa Kilimo ya Uyole – Mbeya,



Mafunzo ya Kilimo Hifadhi kwa wagani kazi na wakulima, kuazisha mashamba darasa ya kilimo hifadhi na urutubishaji husishi wa udongo, mafunzo kwa vitendo kupitia matukio mbalimbali kamavile Nanenane, siku za wakulima na mambo mengine



Akitoa shukrani kwa niaba ya wakulima wenzake Emmanuel Mango kutoka kijiji cha Kitanda Wilaya ya Namtumbo alisema kuwa baiskeri hizo zitawasaidia kwa kiasi kikubwa kuwafikia wakulima katika mambo mbalimbali kwenye maeneo yao



Mango alisema kuwa wadau hao wanatakiwa waisaidie jamii kubwa kwa kuwapa maafisa ugani pikipiki badala ya baiskeli kwani maeneo mengi jiografia yake imekaa vibaya kutokana na kuwa na milima na kuifanya baiskeli kutokuwa nyenzo sahihi ya usafiri kutokana na matumizi mabaya ya muda



Akizungumza kwenye hafla hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Wenseria Swai aliwashukuru wadau wa kilimo hifadhi kwa kazi zao nzuri wanazozifanya na kuwafikia wakulima



Swai alisema kuwa Serikali inatambua wadau hao katika kukuza kilimo bora kwa maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla wake na kwamba serikali itaendelea kuthamini na kuenzi mchango huo muhimu kwa uchumi wa taifa
MWISHO


Chapisha Maoni

 
Top