WAZEE WAKITEMBEA KWA TAABU KWENYE BARABARA YA VUMBI
NA
STEPHANO MANGO,SONGEA
AWAMU
ya nne ya Serikali ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete inaelekea mwishoni kwasababu ifikapo
octoba 25 mwaka huu watanzania watapata fursa ya kuichagua Serikali ya awamu ya
tano kwa mujibu wa Katiba ya Nchi kama ilivyohada yake
Kwa
kutambua hilo octoba mosi mwaka huu ikiwa ni siku 24 mbele kabla ya kufanyika kwa
uchaguzi huo kulikuwa na maadhimisho ya siku ya wazee duniani ambapo wanaharakati
na wazee nchini waliungana na wazee wenzao duniani kuadhimisha siku hiyo muhimu,
nilitamani siku hiyo Rais Kikwete angepata fursa ya kuwaaga wazee hao baada ya
utumishi wake wa miaka 10 kama anavyoaga kwenye maaneo mengine
Na
angesema namna alivyowaaidi wakati anaingia madarakani au alivyokuwa madarakani
ili watanzania wote kwa pamoja wafahamu kipi ambacho alikiahidi kwa wazee na
ametekeleza kipi na anawaachaje katika harakati za kutatua changamoto zao
ambazo kila mara ifikapo octoba mosi ya kila mwaka kwenye maadhimisho yao ya
siku ya wazee duniani walikuwa wanayatoa matamko mbalimbali yenye lengo la
kuboresha ustawi wa maisha yao
Katika
siku hiyo, matamko mbalimbali yamekuwa yakiendelea kutolewa kwa nia ya
kuikumbusha serikali na jamii juu ya wajibu wao katika kuhakikisha kwamba wazee
wanapata haki zao na kuitaka Serikali itemize wajibu wake muhimu wa kuwalinda
na kuwathamini wazee nchini
Kwani natambua
kuwa hadi sasa, masuala mengi mazuri kuhusiana na wazee yamebaki kuwa midomoni
mwa jamii au kwenye nyaraka mbalimbali za serikali na kwamba utekelezaji
kuhusiana na namna ya kumaliza kero za wazee umeendelea kuwa wa chini sana na
matokeo yake, wazee wetu wameendelea kukabiliwa na changamoto nyingi za
kimaisha.
Wazee
wengi wameendelea kulalamika kuwa wametelekezwa na Serikali kwasababu haiwajali
kwenye lishe nzuri, makazi bora,
matibabu ya uhakika na ulinzi madhubuti kwa ajili ya kupata haki yao ya msingi
ya kuishi kama ilivyo kwa Watanzania wengine.
Kwa mujibu
wa Sera ya Wazee nchini, mzee ni mtu mwenye umri wa miaka 60 au zaidi na ripoti
ya sensa ya
watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa kundi hili linahusisha
asilimia 5.6 ya watu wote takriban milioni 45 waliopo nchini.
Na katika muda huo watumishi wa umma na taasisi zake hufikia
umri wa kustaafu ajira zao na wale wasio katika mfumo wa ajira rasmi pia
hufikia hatua ya kupunguza majukumu ya kazi zao kwasababu ya umri, hivyo suala
la uzee na kuzeeka ni dhana inayoelezea hatua ya mwisho ya makuzi ya
binadamu yeyote baada ya kupita katika hatua muhimu za utoto na ujana.
Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali wazee nchini
wanakadiriwa kufikia milioni 5.6 ikiwa ni miongoni mwao ni wazee waliostaafu
ajira katika sekta binafsi na sekta ya umma lakini pia wapo wazee ambao
walikuwa katika ajira zisizo rasmi kama kilimo, uvuvi na uchimbaji madini.
Hata hivyo cha kusikitisha ni kwamba licha ya idadi ya wazee
kuwa ndogo kulinganisha na marika mengine kama vijana, bado wazee wamekuwa
wakikabiliwa na changamoto nyingi zinazotishia ustawi wa maisha yao na hayo
yanatokea, huku taifa likiwa na rundo la
nyaraka zinazozungumzia ustawi wa wazee na namna ya kushughulikia kero zao.
Leo Rais Kikwete anakaribia kuondoka madarakani huku akiwa
ameshindwa kutekeleza Sera ya Taifa ya Wazee ya Mwaka 2003, ambayo inajaribu
kutoa majawabu kadhaa kuhusiana na kero za wazee nchini.
Serikali iliandaa Sera yenye lengo la kutambua changamoto
zinazowakabili wazee, kwa kuwa ilitambua
kuwa wazee ni rasilimali muhimu katika maendeleo ya taifa na ikasisitiza
umuhimu wa kutengwa kwa rasilimali za kutosha kwa lengo la kuboresha huduma kwa
wazee; kuwashirikisha wazee katika maamuzi muhimu yanayowahusu wao na taifa kwa
ujumla na kutoa ulinzi wa kisheria kwa wazee kama kundi maalum, hayo yote
yanaelezwa kwenye aya ya 1.3 ya sera hiyo.
Awamu ya nne inaondoka madarakani huku ikiwa na deni kubwa
ya kushindwa kutekeleza Sera ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2003 na Sheria ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii
ambapo sera ya Taifa ya afya ya mwaka 2007 iliyofanyiwa marekebisho inataja
wazee kuwa ni kundi maalum litakalofaidika na huduma za afya.
Changamoto kubwa ambayo wazee wanakabiliwa nayo ni suala la
matibabu na kuwa licha ya wazee hao kupewa vitambulisho vitakavyowawezesha wao
kutibiwa bila malipo bado mpango huo hauonyeshi tija na kuendelea kuwapatia
usumbufu wazee wetu na kutopata matibabu halisi na kuendelea kusumbuliwa na
maradhi ambayo kimsingi yangepata tiba ya uhakika wazee wangekuwa salama
Licha ya Sheria Na. 1 ya Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii ya
Mwaka 2001, ibara ya 10 (1) inaruhusu Kamati ya Afya ya Kata kuidhinisha wazee
kusamehewa uchangiaji kwenye mfuko huu na kupewa kadi ya utambulisho wa
matibabu bora bila malipo.
Ingawa katika katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ya mwaka 1977, pamoja na marekebisho yake, ibara ya
12 (2) na ibara ya 14, zinazungumzia wazee kupewa heshima na kupata hifadhi
kutoka serikalini na kutoka kwa jamii.
Tamko elekezi la Sera ya Ukimwi inasema Serikali na wadau
mbalimbali wataanzisha mifumo ya hifadhi ya jamii kwa ajiri ya wazee ili
kuboresha uwezo wao katika kukabiliana na madhara yatokanayo na VVU/UKIMWI
jambo ambalo utekelezaji wake unasuasua
Sera ya Taifa ya idadi ya watu na tamko lake elekezi
linahimiza kuanzisha hifadhi za kijamii zinazoshughulikia matatizo ya wazee,
kuhimiza sekta binafsi, asasi zisizokuwa za Serikali na mashiriki ya kidini
kuwekeza katika utoaji wa huduma za kijamii, hususan huduma za afya kwa jamii
lakini mpaka sasa utekelezaji wake ni hafifu
Zipo pia sera nyingine nyingi ikiwemo sera ya taifa ya maafa
ya mwaka 2004, sera ya taifa ya ardhi, sera ya taifa ya hifadhi za jamii ya
mwaka 2003, sera ya lishe na sera zingine zinatamka mahitaji ya wazee lakini
utekelezaji wake umeshindwa kutekelezwa
Pamoja na wingi wa nyaraka zinazozungumzia wazee, viongozi
mbalimbali pia wamekuwa hodari katika kuelezea umuhimu wa ustawi wa wazee kwa
taifa lakini wameshindwa kutekeleza ahadi zao
Akizungumza kuhusiana na serikali kutotimiza kikamilifu
matakwa ya sera na ahadi ambazo zimekuwa zikitolewa na viongozi waandamizi wa
serikali kwenye maadhimisho ya siku ya wazee duniani wilaya ya Songea
yaliyofanyika kwenye viwanja vya Manispaa ya Songea Mkurugenzi wa Shirika
linalohudumia Wazee Nchini PADI Iskaka Msigwa alisema kuwa wazee bado
wanakabiliwa na changamoto nyingi kwani zingine zimeguswa kwa mbali na serikali
lakini zingine bado kabisa hata hajijaguswa
Msigwa alisema kuwa hiyo haimaniishi kuwa serikali haifanyi
chochote yapo ambayo yamefanyika kama
vile kuhakikisha huduma za afya zinapatikana bure kwa wazee wote ingawa pia kuna kasoro nyingi katika hilo,
ingawa juhudi zipo kwa kasi ndogo, lakini nguvu kubwa inahitajika ili angalau
kumaliza nusu ya matatizo yanayowakabili.
“Wazee wengi wamekuwa wakiuawa kikatili kwa imani za
kishirikina, na wakati huo hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa, hali inayozidi
kutia shaka kila siku juu ya wazee wengi waliopo vijijini” alisema Msigwa
Alisema kuwa hali ya upatikanaji wa lishe imefanya afya za baadhi yao kudorora na pia kushambuliwa na maradhi kila mara hali ambayo inatishia uhai wa maisha yao na kwamba suluhisho katika matibabu ya wazee kama bima ya afya ya jamii maana bima itawasaidia hata kwenda kupata dawa katika maduka yaliyoidhinishwa
Alisema kuwa hali ya upatikanaji wa lishe imefanya afya za baadhi yao kudorora na pia kushambuliwa na maradhi kila mara hali ambayo inatishia uhai wa maisha yao na kwamba suluhisho katika matibabu ya wazee kama bima ya afya ya jamii maana bima itawasaidia hata kwenda kupata dawa katika maduka yaliyoidhinishwa
Wazee hao pia wanakabiliwa na matatizo ya kuishi
katika nyumba zilizochakaa zisizo na wavu kwenye madirisha ya kuzuia
mbu, vyoo vya kujisaidia, maji safi ya kunywa na kuoga na kambi
hiyo kukosa umeme kwa muda mrefu.
Kilio kingine cha wazee ni pensheni kwani upatikanaji wake
itampa unafuu wa maisha wa kumudu mambo ya msingi, kwa kuwa wazee nao
walishiriki ujenzi wa taifa kwa namna moja ama nyingine bila kujali alikuwa ni
mfanyakazi katika sekta rasmi au la
Katika maisha ya jamii ya kila siku wazee wanakubalika kuwa ni kisima cha ujuzi katika masuala mbalimbali ya kijamii na pia walitumika katika kutoa mwongozo au ufumbuzi kwa jamii katika masuala muhimu katika nyanja za uchumi, siasa, utamaduni na hata imani.
Katika maisha ya jamii ya kila siku wazee wanakubalika kuwa ni kisima cha ujuzi katika masuala mbalimbali ya kijamii na pia walitumika katika kutoa mwongozo au ufumbuzi kwa jamii katika masuala muhimu katika nyanja za uchumi, siasa, utamaduni na hata imani.
Na kwamba zipo nchi ambazo wazee huheshimiwa sana kutokana
na mchango wao katika jamii husika na hupatiwa mahitaji yote muhimu kama
malazi, mavazi, chakula, uangalizi wa fya zao na ulinzi
Ni muhimu sasa sera ya Taifa ya wazee ya mwaka 2003 ikapitishwa
na kuwa sheria, ili mambo mengi yanayohusu wazee yasimamiwe kisheria kwani yapo
ndani ya Sera hiyo kwani ni jambo la ajabu sana toka mwaka 2003 sera nyingi
zimepitishwa na kuwa sheria lakini haifahamiki ugumu wa sera hiyo kutopitishwa
na kuwa sheria upo wapi.
Ni lazima jamii ikakumbuka kuwa maadhimisho ya mwaka huu ya
siku ya wazee kwa kujielekeza zaidi katika vitendo kushughulikia kero za wazee
na siyo maneno tupu kwani ikumbukwe kuwa vijana wa leo ndiyo wazee wa kesho.
Mwandishi wa Makala haya
Anapatikana 0715-335051
MWISHO
Chapisha Maoni