Charles Mhagama
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
ALIYEKUWA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Mkoani Ruvuma Charles Mhagama katika kipindi kilichopita ameshindwa kutetea
kiti chake cha udiwani wa Kata ya Matogoro kupitia chama cha Mapinduzi baada ya
Mgombea udiwani wa Kata hiyo kupitia chama cha wananchi Cuf Alawi Kawelea
kuibuka mshindi
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Songea Mjini Rafael Kimari alisema kuwa chama
cha Mapinduzi kimefanikiwa kushinda kata 16 na chama cha demokrasia na
Maendeleo (Chadema) kimeshinda kata 4 na chama cha wananchi Cuf kimeshinda kata
1 na kwamba jimbo lote lina kata 21
Kimari aliwataja washindi wa Ccm na kata zao kwenye mabano,
Oddo Mbunda(Mjimwema), Festo Mlelwa(Seedfarm) Mshawej Hassan(Subira) Maurus
Lungu(Mletele) Yobo Mapunda(Lilambo), Lotari Mbawala(Mshangano) Cresensia
Kapinga(Ndilimalitembo)na Osmund Kapinga(Mwengemshindo)
Aliwataja wengine kuwa ni Wilbart Mahundi(Ruhuwiko), Ismail
Aziz(Misufini),Shaib Kitete(Mjini),Hussen Abukadi(Majengo),George
Oddo(Lizaboni),Golden Sanga(Bombambili),Izack Lutengano(Msamala) na Mussa
Mwakaja(Mateka)
Msimamizi huyo alizitaja kata ambazo Chadema imeshinda ni Rashid Msuso(Ruvuma),Mussa
Ndomba(Tanga) Martine Mlata(Matarawe)Seneta Yatembo(Mfaranyaki) na Alawi
Kawelea (Matogoro) ambaye ameshinda kiti hicho kupitia chama cha wananchi Cuf
Alisema kuwa mpaka sasa hajapokea malalamiko yoyote
kuhusiana na matokeo hayo na kwamba hali hiyo inaonyesha kuwa tume ya uchaguzi
imetenda haki yake vizuri na wananchi wametumia haki yao ya kidemokrasia ya
kuchagua kiongozi ambaye wanamtaka
MWISHO
Chapisha Maoni