0

NA STEPHANO MANGO,SONGEA
 
WASHAURI 14 wa mahakama za mwanzo za Mfaranyaki na songea mjini katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamegoma kufanya kazi hiyo baada ya kutolipwa posho kwa miezi mitano.
 
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa masharti ya kutotajwa majina yao washauri hao waliiyambia  TANZANIA DAIMA kuwa tangu mwezi mei mwaka huu hadi sasa hawajapata posho za vikao vya mahakama na wamejaribu kwa muda mrefu wapatiwe posho zao lakini hamna mafanikio.
 
 Walisema kuwa kutokana na hali hiyo wamelazimika kuchukua uamuzi mgumu wa kugoma tangu oktoba 15 mwaka huu na kwamaba hivi sasa wapo majumbani mwao wakisubiri uongozi wa mahakama utachakua hatua gani.
 
Walifafanua zaidi kuwa walikuwa wakiingia gharama kubwa ya nauli ya kutoka majumbani kwao kwenda mahakamani kwa ajili ya kwenda mahakamani kusikiliza kesi mbalimbali lakini posho za vikao vyao wameshindwa kuzipata hivyo wameiyomba serikali kupitia idara ya mahakama kuona umuhimu wa kuwatambua washauri wa mahakama ikiwa ni pamoja na kuhakikisha posho zao kuzipata kwa wakati.
 
Mwenyekiti wa washauri ya mahakama ya mwanzo ya Songea mjini Dominick Njelekela alipohojiwa na TANZANIA DAIMA mwishoni mwa wiki kuhusiana na mgomo alisema kuwa wameamua kwa pamojaa kuto endelea kwenda mahakamani kufanya mambo ya ushauri na badala yake wakisubiri mahakama kama itawalipa posho zao za miezi mitano ilizopita.
 
Njelekela alisema kuwa Mahakama ya mwanzo ya songea mjini inawawashauri wa mahakama 8 na katika mahakama ya mwanzo ya mfaranyaki kunawashauri sita ambao wote kwa pamoja wameamua kugoma mpaka walipwe posho zao.
 
Hata hivyo hakimu Mfawidhi wa mahakama ya mwanzo ya songea mjini Catherine Mattaka alipohojiwa na TANZANIA DAIMA mwishoni mwa wiki ofisini kwake alizibitisha kuwa washauri nane wa mahakama hiyo wamegoma kufanya kazi wakidai kuwa hawajalipwa posho zao lakini alikataa kutoa ufafanuzi zaidi kwa madai kuwa yeye sio msemaji.
 
 
Kwa upande wake mtendaji mkuu wa mahakama kuu kanda ya songea Beatus Benedictusi alipohojiwa na nipashe kwa njia ya simu kuhusiana na mgomo huo wa wawashauri wa mahakama ya mwanzo alikataa kutoa ufafanuazi zaidi na baadaye alikata simu.
 
 
TANZANIA DAIMA haikukata tama ililazimika kumtafuta afisa mtumishi wa mahakama hiyo Brian Haule kwa kumpigia simu yake ya kiganjani na kumtaka atoe ufafanuzi kusiana mgomo wa washauri wa mahakama ya mwanzo ya mfaranyaki na songea mjini naye alizibitisha kutokea mgomo lakini hakutaka kuendele kutoa ufafanuzi zaidi na alidai kuwa atapga simu baada ya nusu saa ili aweze kunifafanulia zaidi lakini hakufanya hivyo na baadaye TANZANIA DAIMA ilirudia tena kumpigia simu zaidi ya mara mbili lakini haikupokelewa.
 
Mwisho.
 

Chapisha Maoni

 
Top