0



KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA RUVUMA MIHAYO MSIKHELA  

NA STEPHANO MANGO,SONGEA



JESHI LA polisi Mkoani Ruvuma imepiga marufuku kwa mtu yeyote au makundi ya watu wa kutoka vyama mbalimbali vya siasa wanaodaiwa kutaka kuandamana kushinikiza kuteuliwa kwa matokeo ya uchaguzi ya ngazi mbalimbali za uongozi (UDIWANI, UBUNGE NA URAIS) yaliyotangazwa hivi karibuni na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mkoani Ruvuma.





Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoani Ruvuma  Mihayo Msikhela alifafanua zaidi kuwa taarifa za ktaka kufanya maandamano baadhi ya watu au makundi toka kwenye vyama vya siasa jeshi la polisi tayari limezipata kupitia vyanzo vya baadhi ya watu waaminifu.



Alisema kufuatia taarifa hizo jeshi la polisi mkoani humo limetoa tahadhari kwa mtu, kikundi cha watu walio na nia hiyo kuwa ni kosa kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kwa mujibu wa kifungu cha 74 cha sheria ya mwenendo ya makoa ya jinai.



Alifafanua kuwa kifungu hicho kinakataza mikusanyiko isiyo halali na kufanya hivyo ni kukiuka sheria hiyo hivyo ni marufuku kwa mtu yeyote au makundi ya aina yoyote toka kwenye vyama vya siasa kufanya mikusanyiko au maandamano ambayo sai halali.



Kamanda Msikhela alisema kuwa jeshi la Polisi mkoani Ruvuma imejipanga kikamilifu kuzuia maandamano haayo na amewataka wananchi wa mkoa huo kutoshawishia  na mtu yoyote kuingia katika maandamano ambayo kimsingi yamelenga kuleta vurugu na kuhatarisha amani iliyopo katika mkoa wa Ruvuma.



Aidha jeshi la Polisi mkoani humo limetoa wito kwa watu au vikundi vinavyoshawishiwa na vyama vya siasa kuona namna ya kutafuta njia nyingine mbadala ya kupata suruhisho kwa mujibu wa sheria hivyo kwa mtu yeyote atakayekutii sheria hiyo atachukuliwa sheria staiki ikiwa ni pamoja na kukamatwa ana kufikishwa mahakamani na si vinginevyo.



MWISHO.




Chapisha Maoni

 
Top