0


NA STEPHANO MANGO, SONGEA

WANANCHI wa kada mbalimbali wametoa maoni yao kuhusu uteuzi, uhamishaji na uenguaje wa wakuu wa Wilaya uliofanyika jana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete na kudai kuwa jambo hilo halikuwa muda muafaka kwa sasa

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mjini hapa walisema kuwa muda uliopo ni wa utekelezaji wa maagizo yake mengi ambayo ameyatoa siku za nyuma hivyo kitendo cha kuwaachisha, kuhamisha na kuteua wakuu wa wilaya wapya kutasababisha kutasababisha kutokutekeleza mipango kazi husika kwasababu wapya watataka kujifunza majukumu yao na kuanza kutembelea maeneo yao ya kazi ili waweze kuyajua na kuanza kupanga mipango yao ya kazi husika

Masumbuko Paulo akizungumza na Gazeti hili alisema kuwa uteuzi na mabadiliko ni muhimu kisiasa lakini kufanya sasa sio muhimu kwa sababu ya mipango ya zamani haitatekelezwa na hawa wapya kwani nao watakuja na mifumo yao ya utendaji kazi

Paulo  alisema kuwa jambo hilo sio la kulifurahia hata kidogo kwani kila yanapofanyika mabadiliko ya uongozi taifa linaingia katika hasara kubwa kutokana na uhamisho,utekelezaji ambavyo wakati mwingine havina tija na hivyo kuendelea kufanya matumizi yasiyo yasababu na kuwabebesha mzigo mkubwa wananchi

Kwa upande wake Isidoli Mdolino Nyati alisema kuwa anampongeza Rais Kikwete kwa uamuzi alioamua kwani amezingatia vigezo kulingana na hali halisi ya mazingira kutokana na changamoto za maeneo husika
Nyati alisema kuwa katika uteuzi huo umefanikiwa kuingiza vijana kwa asilimia kubwa lakini pia amejaribu kuzingatia vigezo vya jinsia kwani ile asilimia hamsini kwa hamsini pia imejitokeza kwa umakini mkubwa

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Askofu James(AJUCO) Denis Mpagaze alisema kuwa uteuzi huo ni wa kisiasa kwasababu hayo yote anayoyafanya ni maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao wa udiwani,ubunge na urais na kwamba haona tija kwa sasa

Mpagaze alisema kuwa wapo wakuu wa wilaya ambao walikuwa wanajihusisha na harakati za watu waliotanga nia ya kutaka kugombea ubunge au urais wamefutwa kazi na wengine wamehamishwa kwa lengo la kudhoofisha kambi husika za kisiasa na kutengeneza ulinzi wake mara baada ya yeye Rais kuondoka madarakani
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top