0

Mkuregenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Sixberth Valentini Kaijage


NA STEPHANO MANGO,SONGEA
MGOMBEA Ubunge jimbo la peramiho wilaya ya songea kupitia chama cha mapinduzi(ccm) Jenister Mhagama ameweka pingamizi la uteuzi la mgombea ubunge wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) katika jimbo hilo Erasmo Mwingira ambaye katika fomu yake imeonyeshwa kuwahaina muhuri wa mahakama na fomu yake haionyeshi kuwa amehapa kwa mahakama gani.
Akizungumza na Mtandao huu jana ofisini kwake  msimamizi wa Tume ya Taifa ya  uchaguzi wa jimbo la Peramiho ambaye pia ni mkuregenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya songea Sixberth Valentini Kaijage  alisema kuwa pingamizi hilo limetolewa jana na mgombea Mhagama   baada ya kugundua kuwa kwenye fomu ya mgombea mwingira ina kasoro.
Alifafanua zaidi kuwa mchakato wa uteuzi wa wagombea ulianza rasmi Agost 8 mwaka huu na siku ya mwisho ya kuwasilisha ilikuwa ni Agosti 21 mwaka huu ambapo kwa jimbo la peramiho kilikuwa na wagombea watatu toka chama cha mapinduzi (ccm) mgombea wake alikuwa ni Jenister Mhagama, Chadema ni Erasmo Mwingira na Democratic party (DP) ni Claudis Haule Claudis.
Alisema kuwa siku ya uteuzi walioteuliwa ni wagombea wawili ambao ni Jenister mhagama wa chama cha mapinduzi (ccm) na Claudis Haule Claudis wa chama cha demokrasia na maendeleo na fomu  majina ya wagombea zilibandikwa kwenye mbao za matangazo lakini mgombea wa ccm jenister alimuwekea pingamizi mwenzake mgombea wa chadema Mwingira ambalo lilipokelewa na msimamizi wa uchaguzi Agost 22 mwaka huu.
Alisema baada ya kupokelewa pingamizi hilo msimamizi wa tume ya uchaguzi ya Taifa jimbo la Peramiho alimjulisha mgombea wa Chadema  Mwingira juu ya pingamizi hilo ili apate nafasi ya kutoa ufafanuzi au maelezo ya pingamizi lilitolewa ndani ya masaa 24.
Alisema katika fomu hiyo iliyowekwa pingamizi mhuri uliowekwa na mahakama sio ule ambao ulikuwa unahitajika na tume ya Taifa ya uchaguzi pia katika fomu yake mgombea  Mwingira  imeandikwa halmashauri ya songea kuweka pingamizi amedai kuwa mgombea mwingira hajaonyesha uhalisia  wa halmashauri anayogombea.
Hata hivyo Mwingira  amesema kuwa yeye aliomba kugombea nafasi ya ubunge kwenye jimbo la peramiho ambalo lipo kwenye halmashauri ya wilaya songea na mhuri ulitumika kwenye fomu yake ni wa mahakama na 

Chapisha Maoni

 
Top