NA STEPHANO MANGO,SONGEA
WATU wawili wamejeruhiwa vibaya
akiwemo askari polisi wa kituo cha polisi cha Lituhi wilayani Nyasa
baada ya gari walilokuwa wamepanda ambalo lilikuwa linasafirisha
mitihani ya darasa la saba kufeli breki na kupinduka .
Kaimu
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Revocatus Malimi alisema kuwa tukio
hilo lilitokea septemba 9 mwaka majira ya saa 12 asubuhi huko kwenye
barabara ya kutoka Darpori kwenda Tingi katika eneo la kijiji cha
mtetema wilayani Nyasa.
Alifafanua kuwa inadaiwa siku hiyo ya
tukio gari lenye namba za usajiri T204 ADC aina ya LAND ROVER 110 ambalo
lilikuwa linaendeshwa na Fulko Ndunguru (29) mkazi wa kijiji cha
Lifakara wilayani Mbinga liliwajeruhi watu wawili ambapo askari H319 PC
Abdallah (25) wa kituo cha Polisi Lituhi na Askari Mgambo Bernad Chanda
(50) mkazi wa kijiji cha Lituhi.
Alieleza zaidi kuwa gari hilo
ambalo lilikuwa limesheheni mitihani lilikuwa linasambaza mitihani ya
darasa la saba kwenye shule za msingi zilizopo kwenye maeneo ya vijiji
vilivyopo wilayani Nyasa liliacha njia na kupinduka na kusababisha
majeruhi hao ambao kwa sasa hivi wamelazwa katika hospitali ya serikali
ya wilaya ya Nyasa iliyopo katika mji mdogo wa Mbambabay.
Hata
hivyo kaimu kamanda wa polisi Malimi alisema kuwa chanzo cha ajali ni
kufeli breki za gari hiyo na kwamba dereva wa gari Ndunguru anashikiliwa
na polisi wakati uchunguzi zaidi wa ajali hiyo ukiwa unaendelea na
kwamba ukikamilika aatafikishwa mahakamani shitaka linalomkabili.
MWISHO
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni