Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Revocatus Malimi
Na Stephano Mango, Songea
WATU watano wamekufa papo hapo na
wengine wawili wamejeruhiwa vibaya na wamelazwa katika hospitali ya mkoa
wa Ruvuma baada ya gari walilikuwa wakisafilia huku likiwa limesheheni
makaa ya mawe kuacha njia na kupinduka kwenye kona za majimaji barabara
ya kutoka songea kwenda njombe katika kijij cha Gumbilo wilaya ya
Songea.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake
kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Revokatus Malimi alilitaja tukio
hilo kuwa lilitokea September 12 mwaka huu majira ya saa 12 jioni katika
kijiji cha Gumbilo nje kidogo ya manispaa ya songea.
Aliwata
walio poteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni Jaffar Ally Hakimu (40)
ambaye alikuwa dereva wa gari hiyo, Sadali Ally ambaye haikuweza
kutambulika umri wake mara mmoja mkazi wa mkoa wa Morogoro, Mwalimu
Gilbert Mbilinyi (42) mkazi wa kijiji cha Mkongotema, Dickson Nyandindi
(32) mkazi wa Mbinga na Mohamed Hald ambaye na umri wake haukutambulika
mara moja wala kabila na hafaamiki ni mkazi wa wapi.
Malimi
aliwataja majeruhi kuwa ni Mussa Muchungwa (40) mkazi wa kijiji cha
mkongotema na Julius Haule (39) mkazi wa kijiji cha Njambe wilayani
nyasa ambaye inadaiwa kuwa alipanda gari hiyo katika eneo la msamala kwa
lengo la kwenda morogoro kuwasalimia ndugu zake.
Alifafanua
zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio gari yenye namba za usajili T 906
CTR aina ya IVECO ambalo lilikuwa na tela lake lenye namba za usajili
T618 CSN mali ya kampuni ya Everlest inayofanya kazi ya kubeba makaa ya
mawe toka kwenye mgodi wa makaa ya mawe uliopo Lwanda wilayani mbinga
kwenda jijini Dar es salaam ambalo lilikuwa linaendeshwa na Jafar Ally
Hakimu likiwa kwenye mwendo mkali liliacha njia na kupinduka kwenye
mfereji uliopo kandokando hiyo na kusababisha vifo vya watu watato
hapopapo na majeruhi wawili.
Kaimu kamanda Malimi alieleza kuwa
chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi ambao ulimsababishia dereva kumudu
usikani wa gari yake kwenye kona kali za majimaji na kupelekea kuacha
njia na kupinduka.
Naye mganga mkuu mfawidhi wa hospitali ya
serikali ya mkoa wa Ruvuma Dr. Philis Nyimbi akiwa kwenye wodi namba 2
ya jinsia ya kiume aliwaambia waandishi wa habari kuwa jana majira ya
saa 2 za usiku wamepokea maiti tano na majeru wawili wa ajali hiyo
ambapo alifafanua kuwa Moses Muchungwa amejeruhiwa mkono wa kulia ambao
unatakiwa ufanyiwe upasuaji na katika maeneo ya kiuno na mgongo
anatakiwa afanyiwe uchunguzi wa kina kwakuwa unaonyesha mifupa miwili
imevunyika, na Julius Haule amepata michubuko na amepooza mkono wake wa
kushoto na mguu wa kulia sehemu ambayo inadaiwa kuwa alishiliwa na
kifusi cha makaa yam awe.
Kwa upande wao majeruhi Muchungwa na
Haule wamewaeleza waandishi wa habari kuwa tangu walipopanda gari hilo
eneo la msamala manispaa ya songea gari hiyo ilikuwa inaenda kwa mwendo
kasi huku dereva na utingo wake walikuwa wanakunywa pombe aina ya bia
jambo ambalo lilisababisha abilia wa gari hiyo walianza kuwalalamikia
lakini abilia walijibiwa kuwa musiogope kufa ni jambo la kawaida
Mwisho.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni