0

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Revokatus Malimi akionyesha jambo
 
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
MAJERUHI wawili wa ajari iliyosababisha vifo vya watano baada ya gari walilikuwa wakisafilia huku likiwa limesheheni makaa ya mawe kuacha njia na kupinduka kwenye kona za majimaji barabara ya kutoka songea kwenda njombe katika kijiji cha Gumbilo wilaya ya Songea wameeleza kuwa chanzo cha ajari hiyo ni ulevi wa kupindukia
 
Wakizungumza na waandishi wa habari jana katika kwenye wodi namba 2 ya majeruhi iliyopo kwenye Hospital ya Serikali ya Mkoa wa Songea majeruhi hao wameeleza kuwa tangu walipopanda kwenye gari hiyo dereva Jaffar Ally Hakimu (40)na utingo wake Sadali Ally ambaye haikuweza kutambulika umri wake mara mmoja  walikuwa wanakunywa pombe kwa fujo jambo ambalo liliwafanya abiria waanze kuwalalamikia
 
Majeruhi Mussa Muchungwa (40) mkazi wa kijiji cha mkongotema  alisema kuwa alianza kumshukuru mungu kwa kumuepusha na kifo katika ajari hiyo ambayo  yeye alikandamizwa na makaa ya mawe mpaka alipokuja kuokolewa  na watu waliofika kwenye eneo la ajari hiyo
 
Muchungwa alisema kuwa akiwa Songea mjini juzi majira ya saa 9: mchana alianza kutafuta usafiri wa kurudi kijijini kwake Matimila na ilipofika saa 11:14 alifanikiwa kupata usafiri wa lori lililosheheni makaa yam awe lakini baada ya kuondoka tu Dereva na utingo wake waliendelea kunywa pombe huku gari likiwa linaendelea na safari
 
Naye majeruhi Julius Haule (39) mkazi wa kijiji cha Njambe wilayani nyasa alisema kuwa  ni mungu tu aliwasaidia kutoka wakiwa hai kwani mabonge ya makaa yam awe yaliwaangukia na ndio hayo hayo ndio yaliowasababishia vifo
 
Haule alisema kuwa kwasasa hivi anasikia maumivu makubwa kwenye mkono wa kushoto na mguu wa kushoto na ameiomba Serikali iangalie namna bora ya kukemea madereva wazembe na kuwachukulia hatua kali za kisheria madereva walevi  kwani wakati wanawalalamikia walijibiwa kuwa nyie mmekuwa wageni wa vifo na kwamba kila mtu atakufa ndipo alipoamua kuhama kutoka mbele na kurudi nyuma
 
Mganga mkuu mfawidhi wa hospitali ya serikali ya mkoa wa Ruvuma Dkt Philis Nyimbi  alisema kuwa hali za majeruhi hao bado sio nzuri na jitihada za madaktari zinaendelea ili kuboresha afya zao na kwamba Moses Muchungwa amejeruhiwa mkono wa kulia ambao unatakiwa ufanyiwe upasuaji na katika maeneo ya kiuno na mgongo anatakiwa afanyiwe uchunguzi wa kina kwakuwa unaonyesha mifupa miwili imevunjika
 
Kwa upande wake Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Revokatus Malimi alilitaja tukio hilo kuwa lilitokea September 12 mwaka huu majira ya saa 12 jioni katika kijiji cha Gumbilo nje kidogo ya Manispaa ya Songea.
 
Malimi alisema kuwa siku hiyo ya tukio gari yenye namba za usajili T 906 CTR aina ya IVECO ambalo lilikuwa na tela lake lenye namba za usajili T618 CSN mali ya kampuni ya Everlest inayofanya kazi ya kubeba makaa ya mawe toka Mbinga kwenye mgodi wa makaa ya mawe uliopo Lwanda wilayani kwenda jijini Dar es salaam ambalo lilikuwa linaendeshwa na Jafar Ally Hakimu likiwa kwenye mwendo mkali liliacha njia na kupinduka kwenye mfereji uliopo kandokando mwa barabara hiyo na kusababisha vifo vya watu watano hapopapo na majeruhi wawili
 
Kufuatia ajari hiyo Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma Malimi amewataka madereva wa vyombo vya moto kuona umuhimu wa kufuata kanuni na taratibu za barabarani sambamba na kuchukua taadhari kwa watumiaji  njia wengine ili kuepuka ajari za mara kwa mara ambazo zinaghalimu maisha ya watu ambao hawana hatia
 
MWISHO


Chapisha Maoni

 
Top