WAHITIMU WAKILA KIAPO CHA UADILIFU
Na Stephano Mango,Songea
VIJANA
1124 waliojiunga na jeshi la kujenga taifa operesheni Kikwete kwa mujibu wa sheria
awamu ya kwanza wamehitimu mafunzo ya miezi mitatu katika kikosi cha 842 KJ
Mlale wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.
Kati
ya vijana hao 1091 wavulana na 1032 wasichana huku vijana 8 wakishindwa
kumaliza mafunzo kutokana na utoro.
Mkufunzi
wa mafunzo hayo Meja Abdusaloom Shausi alisema,kwa muda wote wa miezi mitatu
vijana hao wamejifunza mambo mbalimbali kama uzalishaji mali,sanaa,,mbinu za
kivita,kwata,utimamu wa mwili na huduma ya kwanza.
Aidha,mambo
mengine waliyojifunza ni kuhusiana na kujiepusha na maambukizi mapya ya virusi
vya ukimwi,ufugaji wa nyuki, utengenezaji tofari za kuchoma na mahusiano kwa jamii.
Meja
Shausi alisema,kutokana na mafunzo hayo wanategemea sana vijana watakuwa
waadilifu na waaminifu kwa taifa,wazalendo,heshima na vijana wanaopenda ,kufanya
kazi zao bila ya kusubiri kusukumwa na mtu mwingine.
Naye
Mkuu wa kikosi hicho Meja Thomas Mpuku alisema, lengo la Serikali kurudisha
mafunzo hayo baada ya kusimamishwa mwaka 1994 ni kuwajenga utayari vijana
wanaojiunga na mafunzo kwa mujibu wa sheria na wale wa kujitolea kimaadili,katika maisha yao,nidhamu na
kuwaweka utayari pindi serikali itakapowahitaji.
Mbali
na hilo Meja Mpuku alisema, mafunzo hayo
yatawafanya vijana hao kuwa viongozi wazuri mara watakapopata ajira serikalini
na kwenye taasisi za watu binafsi.
Kwa
Upande wake mkuu wa utumishi katika jeshi la kujenga taifa ambaye alimwakilisha
MKuu wa Jeshi hilo Kanali Menas Mbele alisema,licha ya Jkt kutoa mafunzo ya mbinu za kivita kwa vijana
nchini,hata hivyo jeshi hilo lina
jukumu la kuwaanda vijana katika malezi bora ya kitanzania ili waweze kuipenda
nchi yao.
Alisema,serikali
itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya
kufanya ukarabati na kujenga makambi mapya ili yaweze kuwa na uwezo wa kuchukua
vijana wengi na kuishi katika mazingira mazuri.
MWISHO
Chapisha Maoni