Na Julius Konala,Makambako
CHAMA cha ushirika wa akiba na mikopo cha Mjimwema saccos
kilichopo katika Wilaya ya Makambako mkoani Njombe kimetoa msaada wa branketi
na shuka 100 zenye thamani ya shilingi 810,000 kwa ajili ya kusaidia Hospitali
ya wilaya hiyo.
Mwenyekiti wa chama hicho Bartholomew Sanga,akikabidhi msaada huo kwa mkuu wa mkoa
wa Njombe Dr. Rehema Nchimbi,mwishoni
mwa wiki alisema kuwa saccos hiyo
imeamua kutoa msaada huo baada ya kutambua changamoto mbalimbali zinazoikabili
Hospitali hiyo.
Sanga alifafanua kuwa msaada huo uliotolewa kwa ajili ya
Hospitali hiyo kati yake branketi ni 50 na shuka 50 kwa madai kwamba zimetolewa kwa lengo la
kuwasaidia wagonjwa wanaopangiwa kulazwa hospitalini hapo.
Akipokea msaada huo mkuu wa mkoa wa Njombe Dr.Rehema
Nchimbi,amekipongeza chama hicho kwa msaada wake na kutambua changamoto
mbalimbali zinazoikabili Hospitali hiyo kitendo ambacho amekiita ni cha
kiungwana.
Katika kuguswa na hilo Dr. Nchimbi alichangia kiasi cha
shilingi 100,000 kwa ajili ya kuunga mkono jitihada zilizofanywa na Saccos hiyo
kwa lengo la kusaidia Hospitali hiyo ya wilaya ya Makambako huku akiwaomba watu
wengine na taasisi mbalimbali kuisaidia hospitali hiyo.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa
Makambako Vumilia Nyamoga,ameishukuru na kuipongeza saccos hiyo kwa msaada wake
kwa madai kuwa utasaidia kupunguza changamoto iliyokuwa ikiikabili Hospitali
hiyo na kudai kwamba ofisi yake itaangalia kila linalowezekana kwa ajili ya
kuunga mkono jitiada hizo zilizofanywa na chama hicho katika kusaidia ya wilaya
hiyo.
Wakizungumza muda mfupi mara baada ya kutolewa kwa msaada
huo,baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo walisema kuwa msaada huo
utasaidia kupunguza changamoto za wagonjwa kulala bila ya kujifunika kutokana
na upungufu wa mashuka na branketi.
MWISHO
Chapisha Maoni