0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela



NA STEPHANO MANGO,SONGEA

JESHI la Polisi Mkoani Ruvuma limemtia mbaroni Shukrani Mkingwa (21) Mkazi wa Mfaranyaki Manispaa ya Songea kwa kukutwa na begi  lililosheheni bangi zenye uzito wa kilo 11 ambazo alikuwa akizizafirisha kuelekea mkoani Iringa



Akizungumza jana na Gazeti hili Ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema limetokea Novemba 23 mwaka majira ya saa 12:30 asubuhi huko katika eneo la Mshangano nje kidogo ya Manispaa ya Songea



Msikhela alifafanua kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio Askari Polisi waliokuwa dolia walifanikiwa kumkamata Mkingwa akiwa na bangi ambayo alikuwa amehifadhi kwenye begi tayari kuisafirisha kuelekea Iringa lakini kabla hajaondoka Askari Polisi waliokuwa kwenye eneo hilo walimtilia mashaka pamoja na mzigo aliokuwa ameubeba



Alisema kuwa baadae Askari Polisi walifanikiwa kumkamata na kuanza kumpekua na kukuta bangi kwenye begi lake na alipohojiwa alieleza kuwa anataka kuelekea Iringa na kwamba alikiri kuwa mzigo huo ni wa kwake na pia alionyesha ushirikiano kwa Askari hao kwa kuwapeleka sehemu ambayo ilikuwa ni ghara la kuhifadhi bangi ambayo huwa inasafirishwa maeneo mbalimbali nchini



Alieleza zaidi kuwa Askari Polisi walipofanikiwa kufika kwenye eneo hilo walifanya upekuzi ambapo baada ya kukamilisha walifanikiwa kukamata mifuko mitatu iliyosheni bangi inayokadiliwa kuwa na kilo 19



“Kufuatia tukio hilo mimi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma natoa wito kwa wakulima , wauzaji na watumiaji wa bangi ambayo ni haramu kuacha mara moja na badala yake wajishughulishe na biashara zingine ambayo ni ya halali”alisema Msikhela



Alisema kuwa msako mkali unaendelea wa kuwatafuta waharifu wengine wanaojihusisha na matumizi ya bangi pamoja na wafanyabiasha wa kuuza bangi kwani wananchi wanapaswa kujua kuwa matumizi ya zao hilo yanapelekea kuongezaka kwa matukio ya uharifu hapa nchini

MWISHO


Chapisha Maoni

 
Top