0



NA STEPHANO MANGO,SONGEA
WATU watano wa kazi wa Kijiji cha Mapipili kata ya Kitumbalomo Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma wamelazwa katika Hospitari ya Wilaya ya Mbinga wakiendelea kupatiwa matibabu baada ya kunywa togwa inayosadikiwa kuwa na sumu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 6 mchana huko katika kijiji cha mapipili ambapo aliwataja waathilika wa togwa kuwa ni Edah Kapinga(25), Adelina Nchimbi(23)

Wengine ni Paulina Komba(21) Stamili Mapunda(21) na mtoto mdogo Stella Komba mwenye umri wa mwaka mmoja wote wakazi wa Kijiji hicho ambao bado wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye Hospital hiyo ya Wilaya

Alisema kuwa chanzo cha tukio hilo inadaiwa awali watu hao walikuwa wanakikundi kidogo cha ushirika cha kusaidiana kulima mashamba kwa zamu kwa kila mwanakikundi na siku hiyo ya tukio inadaiwa wanakikundi walialikwa na Edah Kapinga ambaye ni Mlemavu wa ngozi(albino) kwa ajiri ya kumlimia shamba lake kama taratibu za kikundi hicho kilivyojiwekea

Alifafanua kuwa baada  ya kumaliza kulima shamba hilo Edah alikuwa amewaandalia wenzake kinyaji cha aina ya togwa kama shukrani kwa kumlimia shamba na baada ya kumaliza kunywa kinyaji hicho matumbo yao yalianza kuuma na kukimbizwa hospital ya Wilaya kwa ajiri ya matibabu

Alieleza zaidi kuwa kufuatia uchunguzi wa Mganga aliyekwenda eneo la tukio na kuchukua sampuli ya kinywaji hicho inaonyesha kuwa nafaka iliyotumika kutengenezewa togwa hiyo hiyo ilikuwa na sumu ya kuulia wadudu waharibifu wa nafaka

Alisema kuwa kabla ya kutengenezwa togwa hiyo nafaka haikusafishwa kikamilifu hivyo amewataka wananchi wote wakiwemo wakulima kuchukua taadhari kabla ya kupika vinywaji vya kienyeji ili kuepuka madhara yatokanayo na sumu inayowekwa kwenye nafaka
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top