0
              RPC RUVUMA MIHAYO MSIKHELA
Na Stephano Mango, Mbinga


MWANAFUNZI wa darasa la 5 katika shule ya msingi Mahela iliyopo eneo la Ruhuwiko Mbinga mjini Frank Hyera (15) amefariki dunia baada ya kupigwa na jiwe kichwani na mwanfunzi mwenzake.



Akizungumza na www.mangokwetu.blogspot.com jana ofisin kwake Kamanda wa polisi mkoa wwa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea agost 3 mwaka huu majira ya saa saba mchana huko katika mtaa wa Matarawe uliopo Ruhuwiko Mbinga ambako Hyera alipigwa jiwe kichwa na mwanafunzi mwenzake Victor Komba (9).


Alifafanua zaidi kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio Komba anayesoma darasa la 3 katika shule ya msingi Mahela alimpiga jiwe Hyera wakati wanacheza kwenye eneo la shule hiyo.


 Alieleza zaidi kuwa baada ya kutokea tukio hilo Hyera alipoteza Faham na baadaye alikimbizwa katika hosipitali ya srikali ya wilaya ya mbinga kwa matibabu zaidi lakini siku ya kuamkia agost 4 mwaka huu majira ya saa sita na robo usiku mtoto huyo Hyera alifariki Dunia.


Kamanda Msikhela alisema kuwa hata hivyo jeshi la polisi mkoani humo linamshikilia Komba kwa usalama wa maisha yake na upelelezi bado unaendelea kuhusiana na tukio hili.


MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top