0

NA STEPHANO MANGO,SONGEA
WATU wasiofahamika ambao wanadaiwa kuwa ni wafuasi wa vyama vya upinzani wamebomoa mashina mawili ya chama cha mapinduzi CCM pamoja na  kuchana bendera kisha kunyea mavi  na kuyachana mabango ya wagombea  wa chama hicho  yaliyokuwa yamebandikwa katika mtaa wa Makambi kata ya Ndilimalitembo  Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.
 
Akiongea na Mtandao huu jana Katibu wa CCM wa tawi la Makambi  [B],Paris Mauwa alisema tukio hilo limetokea juzi usiku katika eneo hilo baada ya  watu hao kufanya vitendo hivyo vya kubomoa mashina pamoja na kuchana bendera  na mabango.
 
Mauwa alisema kuwa kufuatia tukio hilo chama kilikwenda katika ofisi za polisi na kutoa taarifa ya uharibifu huo na kisha kupata ,RB yenye NA,SONG/IR/4006/2015 ili kufanikisha kuwatafuta wanaofanya vitendo hivyo  vya uharifu maana ni kinyume na sheria za uchaguzi.
 
 Alisema kuwa licha ya kuyachana mabango ya wagombea kuanzia nafasi ya Urais hadi udiwani watu hao walichana bendera na kuwekea kinyesi kwenye bendera jambo ambalo alidai kuwa inaonyesha kuwa ni wafuasi wa vyama vya upinzani kwa kuwa kata hiyo wanashindania watu wa vyama vitatu katika ngazi ya udiwani ambao ni Cresensia Kapinga wa CCM,Leonadi Miholo wa chadema,Yusuphu Kanduru wa ACT Wazalendo.
 
  Baadhi ya wakazi wa eneo hilo ambao hawakutaka kutaja majina yao wakiongea na Mtandao huu walisema kuwa wanasikitishwa na vitendo hivyo ambavyo vimekuwa vikifanywa na  baadhi ya watu kulingana na ukeleketwa wa vyama vyao na kuwafanya wakiuke sheria za   uchaguzi.
 
 Walisema kuwa kuchana mabango ,bendera pamoja na kubomoa  mashina  ya vyama hamanishi kuwa unashawishi ushindi kwenye chama chako bali ni wapigakura ndiyo wenye maamuzi sahihi ya kumchagua mgombea  wanayemtaka.
 
Kwa upande wake kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Revokatus Malimi amesikitishwa na kitendo kilichofanywa na watu wasiyokuwa na nidhamu kwa kuharibu mashina ya chama cha mapinduzi ,kuchana bendera za chama hicho ,mabango na kuweka vinyesi jambo ambalo amedai kuwa ni kosa la jinai hivyo jeshi la polisi kupitia kitengo iterejesia limeanza kufanya msako mkali wa kuwabaini wahalifu hao.
 
    MWISHO.

Chapisha Maoni

 
Top