0
Baadhi ya Viongozi wa Chama cha  Walimu wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya jengo lao
 
NA STEPHANO MANGO,SONGEA

WALIMU kipitia chama chao cha Walimu mkoani Ruvuma (CWT) wamepaza sauti zao kwa lengo la kuunga mkono taarifa ya chama cha walimu  Tanzania (CWT) iliyotolewa na rais wa chama hicho Gratian Mukoba kuhusu serikali kuto tekeleza kwa wakati madai mbalimbali ya walimu na kupuza malalamiko  yao.

Hayo yamesemwa jana na mwenyekiti wa chama cha walimu mkoa wa Ruvuma (CWT) Beno Mwenda wakati akizungumza na waandishi wa habari  mbele ya  watendaji wakiwemo makatibu wa wilaya  na mkoa  kwenye ofisi za chama hicho.

Mwenda alisema kuwa  muundo mpya wa utumishi wa walimu waraka namba mbili wa mwaka 2014 uliwaagiza waajili wote wakiwemo wakurugenzi watendaji wa halmashauri za wilaya na manispaa  kuwaandikia barua watumishi wote wakiwemo walimu za kuonyesha mabadiliko ya majina  ya vyeo kuanzia July 1, 2014.

Alieleza zaidi kuwa katika mkoa wa Ruvuma ni mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya songea ambaye ndiye ametekeleza kwa kuwaandikia walimu wachache japokuwa zinamakosa yanayohitaji marekebisho ambapo wakurugenzi wa wilaya za Songea, Mbinga, Nyasa, Namtumbo na Tunduru wamekaidi kutekeleza maagizo ya walaka huo hivyo kuwafanya walimu wote waichukie serikali yao.

Alifafanua zaidi kuwa walimu wakongwe waliogota TGTS E,F,H na kutopandishwa madaraja ilipofika July 1, 2015 serikali iliahidi kuwapandisha madaraja  walimu wote waliogota july 1, 2015 badala ya july 1, 2014 kama waraka ulivyokuwa unahitaji hivyo kwa mkoa wa Ruvuma hakuna mkurugenzi aliyetengeneza bajeti kwa ajili ya kuwapandisha madaraja walimu hao waliogota TGTSE ni 2608, TGTSF ni 223, TGTSH ni 18 na TGTS1 ni 4 kwa hiyo jumla ya walimu 2855 waliogota  wamenyimwa kupewa madaraja mapya.

Alisema kuwa pia kuwaingiza wakaguzi wakuu wa shule wa wilaya na kanda katika muundo wa mishahara ya viongozi wa serikali na posho ya madaraka kwa wakuu wa shule za msingi, sekondari, wakaguzi wa kata na wakuu wa vyuo vya ualimu serikali ilitoa waraka namba 3 wa mwaka 2014 ulioagiza kwamba utekeleza wake uanze July , 2015 jambao ambalo halijatekelezwa.

Hivyo  mwenyekiti wa chama hicho mkoani Ruvuma Mwenda  ameitaka serikali ihakikishe kuwa madai mbalimbali ya walimu ambayo tayari yamehakikiwa  yalipwe haraka iwezekanavyo na kwamba wakurugenzi wa halmashauri ambao wanadaiwa walitumia fedha zilizotakiwa kuwalipa walimu madai yao wahakikishe kuwa wanazirejesha haraka na kuwalipa walimu husika kabla chama cha walimu(CWT) hakijawachulia sheria kali na serikali pia iheshimu na kutekeleza waraka namba 3 wa mwaka 2014 kuhusu mishahara pamoja na posho ya madaraka pamoja na viongozi wa elimu kwa kuwatambua wakaguzi wakuu wa wilaya, kanda waliopo wenye sifa kuwalipa mishahara viongozi wa serikali LSS(E) na kuwaendeleza wasio na sifa na si vinginevyo
 
MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top