NA
STEPHANO MANGO,SONGEA
WANANCHI
wa Kata ya Matimila Wilaya ya Songea wametakiwa kujitokeza kwa wingi siku ya
uchaguzi wa Wabunge,Madiwani na Rais Octoba 25 mwaka huu ili kuwachagua
wagombea wa nafasi hizo kutoka chama cha Mapinduzi ikiwa ni shukrani kwa
maendeleo waliyoyapata katika sekta mbalimbali nchini
Wito
huo umetolewa jana kwenye Mkutano wa hadhara wa
Kampeni uliofanyika kwenye Kijiji cha Liula, Mpingi na Kikunja na
Mgombea Udiwani wa kata ya Matimila
Menas Komba ambaye pia ni diwani aliyemaliza muda wake wa uongozi katika kata
hiyo
Komba
alisema sababu za wananchi hao kuichagua Ccm zipo wazi hasa kwenye kata ya
Matimila kwani hapo awali barabara nyingi zilikuwa hazipitiki na sasa
zinapitika na madaraja pamoja na vivuko vimejengwa na kuwafanya wananchi
kuendelea na ujenzi wa taifa kupitia shughuli zao mbalimbali za kiuchumi na
kijamii
Alifafanua
kuwa kwa kipindi cha mwaka 2015 na 2020 amejidhatiti kushirikiana na Serikali kufungua barabara
ya Matogoro kwenda Kiheo hadi Liula B,
barabara ya Matimila kwenda Kikunja ili iweze kurahisisha huduma ya usafiri na mawasiliano
miongoni mwa vijiji hivyo
Alisema
kuwa shule za msingi kwenye kata hiyo zilikuwa chache na hazina walimu wa
kutosha lakini leo shule za msingi zipo kwenye vijiji vyote 6 vya kata hiyo na
kwamba walimu wapo wa kutosha hali ambayo imesababisha kila mtoto mwenye umri
wa kuanza shule anapata haki yake ya msingi ya elimu na kufanya kiwango cha
elimu kuwa kikubwa kwenye kata hiyo na hata ufaulu wa kuingia kwenye sekondari
ya kata umekuwa mkubwa sana
Alieleza
kuwa upatikanaji wa huduma ya maji kwenye kata hiyo ni wa asilimia 92 kwa
wananchi wake na kwamba tayari upembuzi yakinifu umeshafanyika kwenye vyanzo
vipya vya maji na fedha zipo kwa ajiri ya kumalizia kazi za kutandaza mipira ya
maji na kuwafanya wananchi hao wanapata maji safi na salama kwa wakati wote
Alisema
kuwa katika kijiji cha Matimila A na B na Kijiji cha Mpangula kuna mradi wa
maji kutoka katika milima ya Matimila mto Kazembe ambao umegharimu milioni 185
ambapo wananchi walichimba mifereji na kufikia mabomba umekamilika na sasa
wanafunga koki kwa ajiri ya kutoa huduma hiyo muhimu
Alifafanua
kuwa katika sekta ya afya kuna zahanati kijiji cha kikunja,liula na matimila
lakini kwenye kijiji cha mpangula ujenzi wake umefikia hatua za kupaua na
kwamba zahanati hizo zina wataalamu wa kutosha pamoja na nishati ya umeme jua
“Changamoto
iliyopo kwenye Zahanati za Kikunja na Liula ni kukosekana kwa wodi za kuwalaza
wagonjwa ambapo kwenye mpango wa 2015 hadi 2020 ni kujenga wodi hizo ,kujenga
Kituo cha afya kimoja ili wananchi waweze kupata huduma muhimu za afya katika
Vijiji vyao badala ya kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu” Alisema Komba
Alisema
kuwa vikundi 35 vya wazee, kina mama na vijana kila kijiji vimewezeshwa na
mfuko wa jimbo fedha za mtaji kwenye shughuli zao za kiuchumi kwenye kaya zao
na kuwafanya waweze kujikimu katika maisha yao ya kila siku
Alieleza
kuwa kata hiyo imefanikiwa kuingia kwenye mpango wa kupata umeme Vijijini(REA)
ambapo katika awamu ya kwanza vijiji vya Liula,Mpangula, Matimila A na Matimila
B na kwamna wananchi wanatakiwa kujiandaa kijasiliamali ili kuweza kunufaika na
nishati hiyo muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi
Alisema
katika kipindi kijacho amejipanga kikamilifu kuisukuma selikari kuhakikisha
wakulima wanapata masoko ya uhakika ya kuuzia mazao yao kupitia bei elekezi ili
kumfanya mkulima aweze kunufaika na kilimo ambacho kimsingi ndio uti wa mgongo
wa wakulima wa kata hiyo
Katika
sekta ya michezo alisema vijiji vyote kumekuwa na mashindano ya Diwani Cup na
kufanikiwa kupata zawadi mbalimbali na kuwafanya vijana kutumia muda mwingi
kwenye michezo badala ya kuingia kwenye makundi mbalimbali maovu hali ambayo
imeifanya kata hiyo kuwa ni kitovu cha amani na upendo
Kwa
upande wake Katibu wa Ccm Wilaya ya Songea Rajab Uhonde alisema kuwa Serikali
ya awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Viongozi
wengine wameweza kuwafikia wananchi katika sekta mbalimbali na kuwafanya
waifurahie Serikali yao
Uhonde
alisema kuwa kwa ushirikiano mkubwa ulioonyeshwa na mbunge wa Jimbo hilo
Jenista Mhagama kuitekeleza vyema ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010-2015
kumeifanya chama hicho kutembea kifua mbele na kuwaeleza wananchi mafanikio
yake
Alisema
kuwa haoni sababu yoyote ya wananchi kuzubaishwa na propaganda kutoka vyama vya
upinzani ambavyo lengo lake ni kufifisha mazuri yaliyofanya kwa kipidhi chote
cha utawala wa serikali zilizopita kwani kila mmoja ni shahidi wa kasi ya
maendeleo yanayotokea kwenye jamii zetu
“Kutoka
na sababu hizo hakuna sababu ya kuiangusha Ccm madarakani bali muda muafaka
umefika wa wananchi kukaa na wagombea na kuweka vipaumbele vyenu ili kuweza
kutafuta kwa pamoja vikwazo ambavyo vinaonekana kurudisha nyuma maendeleo”
alisema Uhonde
MWISHO

Chapisha Maoni