0
MBUNGE MTEULE WA JIMBO LA SONGEA MJINI LEONIDAS GAMA
NA STEPHANO MANGO,SONGEA

CHAMA cha Mapinduzi katika jimbo la Songea Mjini Mkoani Ruvuma Kimefanikiwa kuibuka ushindi wa ubunge baada ya kuhesabu kura mara mbili na kumfanya mgombea wa chama hicho Leonidas Gama kutangazwa mshindi na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo


Akitangaza matokeo hayo Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi wa Jimbo hilo Rafael Kimari alisema kuwa kulikuwa na vyama vitatu ambavyo vilisimamisha wagombea kikiwemo chama cha ACT WAZALENDO,CCM na Chadema


Kimari alimtangaza Leonidas Gama kuwa mshindi kwa kupata kura 40,886, na kufuatiwa na mgombea wa Chadema Joseph Fuime aliyepata 37000 na wa mwisho ni mgombea wa ACT WAZALENDO Emmanuel Msabila ambaye alipata kura 436


Alieleza kuwa katika jimbo hilo idadi ya waliojiandikisha walikuwa ni wapigakura 127738 ambao walitakiwa kupiga kura zao 324 katika jimbo la uchaguzi wa jimbo hilo


Alieleza kuwa jimbo lenye kata 21 chama cha mapinduzi kimefanikiwa kushinda kata 16 , chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanikiwa kushinda kata 4 na chama cha wananchi Cuf kimeshinda kata 1


Awali kabla ya kutangazwa matokeo hayo ya nafasi ya Ubunge wananchi walijitokeza kwa wingi kwenye viunga vya Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kupata matokeo ambayo yalitakiwa kutangazwa majira ya saa 5:00 asubuhi mpaka saa 6:00 mchana kushindikana na kusababisha Jeshi la Polisi kuwataka kutawanyika na wao kukaidi na kusababisha matomu ya machozi kutumika kwa lengo la kuwatawanya


Aidha toka majira ya saa 8:00 mchana barabara zilifungwa na Jeshi la Polisi kutoa amri ya kufunga maduka na biashara zote hali ambayo ilisababisha taaruki kwa wakazi wa manispaa ya Songea


Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kmanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela alisema kuwa wafuasi wa chadema walivumiliwa kwa muda mrefu wakifanya fujo na kuranda randa katikatika ya mji wakishinikiza matokeo yatangazwe bila kufuata utaratibu hali ambayo ilailazimu Askari kutumia mabomu kuwatanya na kupisha utangazaji wa matokeo hayo

MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top