JUMLA
ya vituo 216 vimetengwa kwenye jimbo la Peramiho lililopo katika Halmashauri ya
wilaya ya Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya kupigia kura katika uchaguzi mkuu
ujao utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Akizungumza
na gazeti hili ofisini kwake jana kwa niaba ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo
hilo Sixbert Valentine,Afisa uchaguzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Furaha
Mwangakala,alisema maandalizi kwa ajili ya uchaguzi huo yamekamilika.
Mwangakala
alifafanua kuwa katika kila kituo kutakuwa na wapiga kura 450 kwa lengo la
kupunguza msongamano na kutoa fursa kwa wananchi wote wa jimbo hilo
waliojiandikisha waweze kupiga kura bila ya kupata adha yeyote.
Aidha
alisema kuwa kufuatia zoezi hilo jumla ya watu 67,334 wa jimbo la Peramiho
wenye sifa ya kupiga kura wamejiandikisha miongoni mwao yakiwemo makundi maalum
mbalimbali ya wazee,vijana wanawake kwa wanaume kwa ajili ya kutumia haki yao
ya msingi ya kuwachagua viongozi wao.
Hata
hivyo alieleza kuwa kwa upande wa maandalizi kwa ajili ya uchaguzi mkuu
yanaendelea vizuri kwa madai kuwa mpaka sasa jumla ya wasimamizi wa uchaguzi
800 wameteuliwa,maboksi ya nyongeza ya bluu 40,meusi 40 na meupe 40 tayari
yamekwisha wasili.
Afisa
uchaguzi huyo aliendelea kuvitaja vifaa vingine vilivyowasili kuwa ni mabango
ya hadhari,mabango ya vituo,mabango yamshale,nyembe za kukatia lakili,betrii za
taa,vitabu vya maelekezo kwa watakaosimamia uchaguzi pamoja na fomu kwa ajili
ya mafunzo ya wasimamizi wa vituo na makarani.
Mwangakala
aliongeza kusema kuwa kwa upande wa makundi maalum hususan kwa watu
wasioona tayari wamekwisha waandalia karatasi maalum za kupigia kura pamoja na
kuwatengenezea utaratibu mzuri wazee na akina mama wajawazito katika
kupiga kura ili wasisimame kwa muda mrefu vituoni kwa lengo la
kuwaondolea uchovu
Hata
hivyo baadhi ya wananchi wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili
walisema kuwa wanashindwa kuelewa kutokana na matamko mbalimbali yaliyotolewa
yakiwemo ya baadhi ya vyama vya siasa kuwaambia wafuasi wao kuwa wakipiga kura
lazima wazilinde,sheria ya tume inasema piga kura kisha simama umbali wa mita
100 na vyombo vya dola vinasema piga kura rudi nyumbani hivyo hawaelewi wafuate
ipi.
MWISHO
Chapisha Maoni