WAPIGA KURA nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupiga
kura na kuzilinda mpaka matokeo yatangazwe na mamlaka husika kwenye vituo vyao
ili waweze kujua hatma ya wagombea wao kwenye ngazi ya udiwani na ubunge nchini
Wito huo umetolewa jana na mke wa mgombea Urais kupitia
umoja wa katiba ya wananchi(UKAWA) Regina Lowassa kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika kwenye viwanja wa wazi vilivyopo kata ya Bombambili katika
halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma
Regina alisema kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1995,2000,2005
na 2010 wapiga kura walilinda kura zao kwa amani na utulivu hata hivyo kwenye
uchaguzi wa mwaka 2015 kwa kutumia utaratibu kama wa awali na kwa sheria
zilizile wanatakiwa kulinda kura zao bila kuingiliwa na mamlaka yoyote ya dola
kwani kura hizo ni haki ya wananchi na sio mali ya Serikali
Alisema kuwa wananchi kwa kulinda kura zao wataondokana na
fikra za hofu ya gori la mkono ambalo limekuwa likitamkwa na viongozi
waandamizi ndani ya chama cha mapinduzi (Ccm) na badala yake wajitokeze kwa
wingi kupiga kura na kuzilinda mpaka matokeo yatangazwe
Alifafanua kuwa wananchi wengi wanataka mabadiliko ya dhati
ya kimfumo na kimaendeleo hivyo ni muhimu kutumia haki ya kidemokrasia
kujitokeza na kupiga kura ili kupata viongozi makini kutoka kwenye Ukawa kwa
maendeleo ya watanzania kiujumla
“Nawaomba akina mama wenzangu tushirikiane kikamilifu
kufanya mabadiliko ya kweli katika uchaguzi wa mwaka huu ili tuweze kuzijenga
familia zenye misingi bora ya kiafya, kielimu, kimiundombinu, kiuchumi na
kiutawala ili tuwatendee haki vizazi vijavyo” alisema Regina
Alisema kuwa hakuna mtanzania ambaye haelewi uadilifu na
uchapakazi wa Edward Lowassa kwenye nafasi mbalimbali alizopata kushika huko
nyuma na namna wagombea wa Ukawa walivyokuwa wachapakazi hivyo ni vyema wagombea
hao wakatendewa haki ya kuchaguliwa ifikapo octoba 25 mwaka huu ili waweze
kutuletea Tanzania mpya
Kwa upande wake mgombea ubunge wa Jimbo la Songea Mjini
kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Joseph Fuime aliwaomba
wananchi wamsaidie kwa nguvu zote kuwapigia kura wagombea wanaotokana na ukawa
ili iwe lahisi kufanya nao kazi kwani kwenye kata nyingi za jimbo hilo
wameonyesha nia ya kuwachagua wagombea wa ukawa
Fuime alisema kuwa kura zikiwa nyingi hata kama wataiba bado
ushindi utapatikana kwa wagombea wa Ukawa kwani wamekuwa na dhamira ya dhati ya
kutatua changamoto za jimbo hilo na kwamba kwa upande wa mgombea urais Edward
Lowassa ambaye ni kipenzi cha watanzania yupo tayari kupambana na umaskini na
mifumo chakavu ya elimu
Naye Mgombea Ubunge wa Jimbo la Namtumbo kupitia chama cha
Wananchi (CUF) Bonifansia Mapunda alisema kuwa wananchi wa jimbo la Namtumbo
wako tayari kwa mabadiliko na wagombea wote wa ukawa wanatosha hivyo wananchi
wasipoteze muda wao kusikiliza propaganda za Cccm
Mapunda alisema kuwa wapiga kura watumie haki yao ya msingi
kuwapigia kura ili waweze kuleta mabadiliko ya kweli kwani sie maneno kidogo na
kazi zaidi hivyo tambo za Ccm za kupiga push up na maneno ya kejeri kwa
wagombea wa ukawa hayana nafasi yoyote katika ushindi
Alisema kuwa wanachokifanya wanaukawa ni kutengeneza ushindi
uliodhahiri kwani wamechoka na ahadi hewa huku wananchi wakiendelea kuteseka na
kuburuzwa zaidi ya miaka 50 ya uhuru bila kuonja matunda yatokanayo na uhuru
Awali Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chadema(Bawacha) mkoa
wa Ruvuma Mariam Mtamike akifungua mkutano huo alisema kuwa wanawake wa chadema
kwenye uchaguzi wa mwaka huu wako makini kuhakikisha ushindi unapatikana kwa
wagombea wa ngazi zote kwenye mkoa wa Ruvuma
Mtamike alisema kuwa kwa kipindi kirefu Ccm imekuwa
ikiwaonga akina mama chumvi, kofia, vilemba na furana bila kuwapa viatu au
mboga za kuungia hiyo chumvi hivyo tumechoka na ulaghai wao na sasa tunatembea
kifua mbele tukiyafuata mabadiliko
MWISHO
Chapisha Maoni