MIONGONI MWA WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI GEOFREY NILAI
NA STEPHANO MANGO,SONGEA
WAJUMBE
wanne wa kamati ya utendaji wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa
Ruvuma(RPC) wamejiudhuru nafasi zao kutokana na mwenendo mbaya wa
uongozi ukiwemo ubadhirifu wa mamilioni ya fedha za chama na matumizi
mabaya ya madaraka ya viongozi wakubwa wa chama hicho
Akizungumza
mbele ya waandishi wa habari jana kwenye ukumbi wa hotel ya OK mmoja wa
wajumbe wa kamati ya utendaji waliojiudhuru Geofrey Nilai aliwataja
wajumbe wenzake kuwa ni Kassian Nyandindi, Joseph Mwambije na Mpenda
Mvula na kusema kuwa kwa umoja wao wamejiudhuru nafasi zao ndani ya
chama kuanzia machi mosi mwaka huu na watabaki kuwa wanachama wa kawaida
Nilai
alisema kuwa wameamua kujiudhuru nafasi zao kwa manufaa ya chama ambapo
alitaja mambo yaliowafanya wafikie hatua ya kujiudhuru ni pamoja na
kutofanyika kwa vikao vya kamati ya utendaji kulingana na katiba ya
chama,kutotolewa taarifa za fedha za chama kwa kipindi cha miaka mitatu
na toka ufanyike kwa uchaguzi mkuu wa chama mwaka jana hakuna kikao
kilichofanyika cha kukabidhiana mali za chama
Alisema kuwa sababu
nyingine ni mwenyekiti wa chama hicho Andrew Kuchonjoma kushindwa
kuitisha kikao cha kubadilisha watia sahihi kwenye akaunti za chama
zilizopo benki na badala yake anatumiwa mwanachama wa kawaida ambaye sio
kiongozi jambo ambalo ni kinyume na katiba ya chama na ushirikishwaji
mdogo wa masuala ya chama kwa wajumbe wa kamati ya utendaji,pia kamati
ya utendaji kutokabidhiwa vifaa vinavyotolewa na muungano wa klabu za
waandishi wa habari nchini(UTPC)
Alieleza zaidi kuwa sababu
nyingine ambayo imewafanya wajiudhuru ni kutoshirikishwa mradi wa redio
ya chama licha ya kuwa kuna tetesi ya manunuzi ya vifaa vya redio hiyo
lakini wajumbe wa kamati ya utendaji mpaka tunafikia uamuzi wa
kujiudhuru mwenyekiti Kuchonjoma ameshindwa kuwaonyesha na kueleza
thamani ya vifaa hivyo na kikao kilichomwagiza kwenda kuvinunua
Alisema
kuwa sababu nyingine ni kufunguliwa kwa akaunti benki kwa ajiri ya
maafa kwa waandishi wanachama wa RPC bila kuwashirikisha wanachama
wenyewe pamoja na kamati ya utendaji, pia ilichangishwa michango kwa
wadau mbalimbali kwa ajiri ya mradi wa redio lakini hakuna taarifa ya
fedha iliyotolewa kwenye kamati ya utendaji juu ya fedha hizo
Alisema
kuwa kutokana na sababu hizo kwa umoja wetu tumefikia uamuzi wa
kutokuwa na imani na viongozi wakuu wa chama hicho na kwa hiali yetu
tumeamua kujiudhuru nafasi hizo ili wanachama wapate fursa ya kuitisha
uchaguzi mkuu mpya ili kuweza kupata viongozi bora ambao watafuata
katiba ya chama na misingi ya utawala bora na tayari barua ya kujiudhuru
tumeuandikia uongozi wa chama hicho na nakala ya barua hizo zimepelekwa
muungano wa klabu za waandishi wa habari Tanzania(UTPC) na Baraza la
Habari Tanzania (MCT) kwa taarifa za jambo hilo
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Ruvuma Andrew
Kuchonjoma alipoulizwa kuhusiana na wajumbe wa kamati ya utendaji
kujiudhuru, alikiri kupokea barua kutoka kwa wajumbe wake wa kamati ya
utendaji ambao wamejiudhuru nafasi zao ndani ya chama
Kuchonjoma
alisema kuwa kwa kuwa wao wameamua kuchukua maamuzi magumu ya kujiudhuru
nyadhifa zao kwa hivi sasa wajumbe waliobakia kwa maana ya mwenyekiti,
makamu mwenyekiti, mweka hazina na mweka hazina msaidizi wanaandaa
mkutano maalumu wa uchaguzi wa kujaza nafasi za wajumbe waliojiudhuru
MWISHO
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Chapisha Maoni