0


       Emmanuel Mlaponi akiwa na mama yake mzazi

NA STEPHANO MANGO,SONGEA


MTOTO Emmanuel Mlaponi (16) akiwa na wadogo zake wane na mama yake wamemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuri kuona umuhimu wa kuingilia kati sakata la kupatikana kwa mirathi ya baba yake aliyepotea tangu mwaka 2005


Akizungumza na gazeti hili jana Emmanuel Mlaponi ambaye yupo kidato cha pili alisema kuwa yeye na mama yake wamekuwa wakiishi maisha ya taabu sana toka baba yake ambaye alikuwa anafanya kazi katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma alipopotea mwaka 2005


Kijana huyo anasema kuwa yeye na mama yake walipoona kuwa Benedict Mlaponi amekata mawasiliano na ameshindwa kurudi walijitahidi kwenda ofisini kwake kumuulizia bila mafanikio yoyote huku miaka inaenda ndipo walipofungua mirathi yam zee huyo ili waweze kunufaika na jasho lake


Alisema kuwa mirathi ilifunguliwa na Serikali iliridhia tupewe haki  ya mzee wetu lakini mpaka sasa hatujapata na hatujui kama ilichukuliwa au ndiyo majipu yanayo tumia fedha za wajane na ndio maana sasa tunatapatapa ili tuweze kulipwa stahiki yetu


Naye mke wa Benedict Mlaponi aliyejitambulisha kwa jina Angetruda Millinga akisimulia mkasa huo anasema kuwa mume wake alikuwa mfanyakazi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Songea na kwamba alipotea toka 13/10 /2005 mpaka leo hajulikani alipo. 


Millinga anasema kuwa mara ya mwisho mume wake aliaga kuwa anasafiri kikazi kwenda jijini Dar es salaam na alipata ruhusa kutoka kwa mkuu wake wa kazi wakati huo alikuwa Dkt Wella hivyo toka wakati huo mpaka leo 2016 hajapatikana na haijulikani kama yuko hai au amekufa na kuwaacha watoto wake watano pamoja na mimi ambaye ni mke wake wa ndoa


Mama huyo anasema mkuu wake wa kazi alipoona mtumishi wake hayupo kazini kwa zaidi ya miezi 6 bila taarifa yoyote na bila kujua tatizo lilompata masikini wa Mungu Benedict Mlaponi aliandikiwa barua ya kufukuzwa kazini 


“Mimi na familia tukashauliana namna ya kufanya ndipo tukapitisha pombe ya mila na kuhesabu kuwa mume wangu amekufa na tukaenda kutoa taarifa katika kituo kikuu cha Polisi kilichopo Songea na tufungua kesi ya mirathi”alisema Millinga


Alisema baada ya kutoa ripoti polisi na kuona hapatikani Mahakama ikaamuru mimi na familia ya watoto watano tulipwe fedha ya mirathi lakini Serikali ya Mkoa wa Ruvuma haijaweza kufanya hivyo hadi sasa. 


Alisema anawaomba wanaharakati mbalimbali waweze kumsaidia kupata mirathi hiyo kwani amekuwa akiteseka sana kuwalea watoto hao pekee yake toka mwaka 2005 hadi leo kwani naanza kukata tama ya kupata haki ya mume wangu


Mume wangu alikuwa akifanya kazi Serikalini kwa nini asilipwe mafao ya mirathi wakati kesi ilishapitia na kuthibitika kuwa mume wangu kafariki katika mazingira ya kutatanisha ,hivyo namuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Magufuli anisaidie kwani nimeshakuwa mjane na familia inanitegemea na  hajulikani fedha imeingia mikononi mwa majipu

MWISHO

Chapisha Maoni

 
Top