Na Gideon Mwakanosya-Songea
MFUKO wa Pension wa jamii( PPF) kama
ilivyo moja ya majukumu ya mfuko huo umetoa elimu kwa wananchi wenye
ulemavu wa kuto kusikia( Viziwi) 50 ambao wamepata elimu kuhusu hifadhi
ya jamii na umuhimu wa kujiwekea akiba ya baadaye.
Hayo yalisemwa
na meneja wa kanda ya kusini wa mfuko huo wa PPF Kwame Temu wakati
alipokuwa akitoa elimu jinsi namna ya kuweka akiba kwenye mfuko huo wa
pension wakati Mwananchi akiwa kwenye shughuli zake mbalimbali za kila
siku zikiwemo za ujasiliamali .
Alieleza kuwa wote Scheme ni
mfumo maalum wa kuchangia unaohusisha sekta isiyo rasmi pamoja na ule
mfumo wa ziada uliopo kwenye mfumo wa sekta iliyo rasmi hivyo lengo la
mfumo huo wa wote scheme ni kukidhi mahitaji na kutambua mchango na
ushiriki wa sekta isiyo rasmi kwenye uchumi na pia kutoa fursa
mbalimbali kwa wajasiliamali pamoja na waendesha bodaboda.
Alieleza
zaidi kuwa mfuko huo wa PPF ulikuwa umeandaa semina kwa ajili ya kuwapa
elimu walemavu wasiosikia( viziwi) ambao wengi wao wapo katika mfumo
usio rasmi kwa kuwapa elimu jinsi ya kujiunga na kulindwa na mfuko wa
jamii pamoja na kufaidika na mafao mbalimbali kupitia mfuko huo.
Temu
alitaja mafao yanayotolewa na PPF kuwa ni Afya kwa ajili ya kujali afya
ya mwanachama wa PPF, Fao la uzeeni, Mkopo wa Elimu na mkopo wenye
lengo la kutimiza ndoto ya mwanachama ambapo washiriki baada ya kuelewa
umuhimu wa mafao hayo walijiunga na mfuko huo na kwamba semina hiyo
ilikuwa na mafanikio makubwa.
Kwa upande wake Katibu mkuu
mtendaji wa Taasisi ya Maendeleo ya Viziwi Tanzania (TAMAVITA) Kelvin
Nyema akichangia mada kwenye semina hiyo aliwaomba wabunge wa majimbo ya
Peramiho, Madaba na Songea Mjini mkoani Ruvuma waone umuhimu wa
kuwasidia walemavu viziwi kuchangia angalau kwa kipindi cha miezi 6 kwa
kila mmoja kama walivyoahidi kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka
jana.
Nyema alieleza kuwa jinsi ya kuchangia kwa kiwango cha
chini kuchangia kwa mwezi ni shilingi elfu ishirini(20,000/) ambacho
kinawezwa kulipwa aidha moja kwa moja kwenye akounti ya mfuko wa
Pension wa PPF au kwa njia ya simu za mikononi za makampuni ya Vodacom
(M-Pesa), kampuni ya AIR TEL (AIR TEL MONEY) na Kampuni ya TIGO( TIGO
PESA) hivyo wabunge bado wanaombwa kuwasaidia walemavu viziwi ambao
wamekuwa wakijishughulisha shughuli mbalimbali za ujasiliamali badala ya
kupita mitaani kuomba .
MWISHO
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni