MKE WA MGOMBEA URAIS EDWARD LOWASSA , MAMA REGINA LOWASSA
MGOMBEA WA UBUNGE JIMBO LA SONGEA MJINI JOSEPH FUIME AKIENDELEA KUWAOMBA KURA WANANCHI
NA STEPHANO MANGO, SONGEA
MKE wa mgombea Urais kupitia umoja
wa Katiba ya Wananchi(UKAWA) Regina Lowassa anatarajia kuhutubia maelfu ya
wananchi wa Manispaa ya Songea na vitongoji vyake kesho(leo) kwenye kiwanja cha
wazi kilichopo kata ya Bombambili Katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Akizungumza na waandishi wa habari
jana Ofisini kwake Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema Mkoa wa Ruvuma (Bawacha)
Mariam Mtamike alisema kuwa Regina Lowassa akiwa ameambatana na Naibu Katibu
Mkuu wa Bawacha Taifa Kunti Majara na viongozi wengine toka makao makuu ya
Chadema atafanya mkutano mkubwa kuanzia majira ya saa 5:00 asubuhi mpaka majira
ya saa 11:15 na baada ya hapo ataelekea Mkoani Mbeya kwenye mikutano mingine ya
Kampeni
Mtamike alisema kuwa lengo la
mkutano huo ni kuwanadi wagombea Urais,Ubunge na Madiwani wa Ukawa na
kuzungumza na wanawake wa Wilaya ya Songea wawe na ujasiri wa kufanya
mabadiliko ya kuwachagua wagombea hao ili kuyafikia malengo stahiki
Alisema kuwa Chadema Mkoa wa Ruvuma
wamejipanga kikamilifu katika kuhakikisha kuwa ushindi wa kishindo unapatikana
kwa wagombea wa ukawa kwani kwasasa wanawake wanaendelea na mikakati ya ushindi
ikiwemo kupita nyumba kwa nyumba kuwanadi wagombea wao na kuwahamasisha wananchi
wajitokeze kwa wingi siku ya uchaguzi Octoba 25 mwaka huu na kuwachagua
wagombea wa Ukawa kwa nafasi ya Udiwani, Ubunge na Urais
“Naziomba mamlaka zinazohusika
ikiwemo Tume ya Taifa ya Uchaguzi iwaache wananchi wapige kura kwa uhuru ili
watimize haki yao ya kimsingi ya kupiga kura kwa wagombea ambao wanawahitaji
kwani kuendelea kusuka hujuma kutaleta vurugu ambazo zitaharibu amani, na hata
haki ya wapiga kura hao kulinda kura zao isichezewe” alisema Mtamike
Alisema kuwa wananchi wanatakiwa
kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano huo ili waweze kupata ujasiri wa kupiga
kura na kulinda kura zao siku ya uchaguzi ili kuweza kufanya mabadiliko ya
dhati ya kiuongozi mwaka huu
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) John Mwankina alisema kuwa kuna taarifa za
uchakachuaji ambazo wamezibaini na kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzifanyia
kazi haraka iwezekanavyo ili kuufanya uchaguzi uwe wa haki
Mwankina alisema kuwa idadi halali
ya wapiga kura jimbo la uchaguzi la Songea Mjini ni 127,719 lakini imeonyesha
kuwa wapigakura waliozidi ni 1122 hivyo tumeiandikia tume barua yenye
kumbukumbu namba CDM/SMJ/10/2015/17 ya tarehe 13/10/2015 ili iweze kutoa ufafanuzi wa kina wa idadi
halali ya waliojiandikishe kupiga kura ili kuondoa dosari katika uchaguzi wa
jimbo hilo
Alisema kuwa Chama cha Mapinduzi kwa
kushirikiana na Serikali imekuwa ikihangaika kuwafanyia hujuma mbalimbali
wagombea wa Ukawa wa nafasi ya Udiwani na Ubunge hali ambayo inatutia shaka na
kuwapa hofu wananchi kwenye mchakato mzima wa kampeni na kuelekea uchaguzi
MWISHO
Chapisha Maoni