NA STEPHANO MANGO,SONGEA
MAMA mmoja aliyefahamika kwa jina la Amaliya Mikael Mbawala (91) mkazi wa kitongoji cha
Liula A Kijijini Liula kata ya Matimila wilaya Songea mkoa wa Ruvuma amefariki dunia baada ya kuumwa na nyuki kwenye eneo la Makaburi wakati wa mazishi ya Mtoto wake Sixmund
Komba (60).
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa tukio hilo lilitokea februari 13 mwaka huu majira ya
saa 9:30 alasiri huko katika kitongoji cha Liula A mara baada ya kiongozi wa Kanisa Katoliki ambaye pia ni Naibu Askofu Camilius Haule kubariki kaburi na jeneza kushushwa na kuanza kuwekwa udogo kwa ajiri ya kufukia kaburi ndipo nyuki ambao walikuwa kwenye mti mita chache karibu na kaburi walianza kuwashambulia waombolezaji
MAMA mmoja aliyefahamika kwa jina la Amaliya Mikael Mbawala (91) mkazi wa kitongoji cha
Liula A Kijijini Liula kata ya Matimila wilaya Songea mkoa wa Ruvuma amefariki dunia baada ya kuumwa na nyuki kwenye eneo la Makaburi wakati wa mazishi ya Mtoto wake Sixmund
Komba (60).
Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa tukio hilo lilitokea februari 13 mwaka huu majira ya
saa 9:30 alasiri huko katika kitongoji cha Liula A mara baada ya kiongozi wa Kanisa Katoliki ambaye pia ni Naibu Askofu Camilius Haule kubariki kaburi na jeneza kushushwa na kuanza kuwekwa udogo kwa ajiri ya kufukia kaburi ndipo nyuki ambao walikuwa kwenye mti mita chache karibu na kaburi walianza kuwashambulia waombolezaji
Walisema kuwa hali hiyo iliwafanya waombolezaji na viongozi wa dini ambapo walikuwa maparoko
watatu wakiongozwa na Naibu Askofu wa Haule na masista walitimka mbio na
kuliacha kaburi likiwa wazi na kutokomea pande mbalimbali za makaburi hayo kwa
lengo la kujiokoa na mashambulizi ya nyuki hao
Walieleza kuwa katikati ya januari mwaka huu wakati
wanamalizia kuzika kundi la nyuki lilivamia makaburi hayo lakini hawakuleta
madhara yoyote kwani walizunguka kwa dakika chache kasha walirudi kwenye eneo
la makazi yao yaani kwenye nyumba yao maarufu kwa jina la masega
Walisema pia mwanzoni mwa februari mwaka huu wakati wanazika
msiba ungine nyuki mmoja alijitokeza makaburi na kumng’ata muombolezaji mmoja
na kuondoka zake lakini katika msiba wa Sixmund Komba hali hiyo ni tofauti
“Tumeshtushwa sana kutokana na kundi hilo la nyuki
kuwashambulia waombolezaji kwa kasi na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia na
watu wanne kupumzishwa kwenye zahanati ya kijiji cha Liula na waombolezaji
wengine kujeruhiwa kutokana na nyuki hao” alisema Norasco Mapunda ambaye ni
Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho
Mapunda alisema kuwa kutokana na tukio hilo wapo watu ambao
wanahisi kuwa kuna ushirikina ndani yake lakini yeye alimfahamu marehemu na
kwamba alikuwa anakaa nae karibu hivyo wananchi wanapaswa kupuuza maneno hayo
Alisema kuwa mara baada ya tukio hilo kutokea watu wanne
usiku walirudi makabulini kwa ajiri ya kufukia kaburi na kuukata mti ambao
nyuki walikuwa wakiishi pamoja na kuwachoma moto nyuki hao kwa kutumia mafuta
ya taa na petrol
Alieleza kuwa siku ya pili yake ilikuwa ni siku ya mazishi
ya Bibi Amaliya Mbawala watu wachache walijitokeza makaburini kwa ajiri ya
kuchimba kaburi lake na kuhakikisha nyuki wote wameuawa ili kupisha mazishi
hayo na kusawazisha kaburi la Sixmund ambalo lilifukiwa jana yake usiku
Akizungumza kwa niaba ya familia mtoto wa mwisho wa Bibi
Amaliya , sista Skolastika Komba alisema kuwa katika mazishi hayo ambayo
yalikuwa na ukimya mwingi ambapo wazee walizuiliwa kwenda makabulini ,huku tu
ambao wakiwa na vikinga mashambulizi ya nyuki walifanikiwa kuzika salama na
ndugu na majamaa kupata nafasi ya kuweka misalaba kwenye makaburi yote mawili,
kuweka mataji,kuwasha mishumaa na kubari makaburi yote mawili
Komba alisema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo
cha mama yake na kwamba katika familia walikuwa sita na sasa wanabaki watano
wakiwa hawana baba wala mama licha ya kuwa jitihada za kumuokoa mama yake zilishindikana
kwani wakati anajaribu kumuokoa yeye na wenzie makabulini hapo walingatwa sana
na nyuki na kusababisha maumivu makali katika miili yao nay eye kupoteza
kilemba cha usista wake alichokuwa amekivaa kwani nyuki waliingia kwenye kichwa
chake na kumng’ata sana na kumsababishia manundu mengi
Kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Zuberi Mwombeji amethibitisha
kutokea kwa tukio hili na kwamba Februari 14 alifika eneo la tukio na kufanya
mahojiano na mashuhuda mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali na ndugu za
marehemu
Akizungumza na gazeti hili eneo la tukio juzi Kamanda
Mwombeji alisema kuwa inadaiwa siku hiyo ya tukio kulikuwa na mazishi ya Sixmundi
Komba ambaye katika uhai wake alikuwa ni mwanajeshi mstaafu wa Jeshi la
wananchi Tanzania (JWTZ) kikosi cha Nachingwea ambapo baada ya kustaafu inadaiwa aliamua kuishi
Liwale Mkoani Lindi ambapo baadaye alipatwa na maradhi ya muda mrefu na alifariki
dunia.
Alieleza kuwa komba baada ya kufariki dunia jitihada zilifanywa za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka Liwale hadi kijijini Liula nje kidogo ya Manispaa ya Songea ambako walifika majira ya usiku wa kuamkia Jumamosi ya februari 13 mwaka huu.
Alisema kuwa baada ya kuufikisha mwili wa marehemu kijijini hapo taratibu za mazishi ziliendelea ambapo majira ya 9:30 alasiri wananchi wa kitongoji hicho wakiwemo wafiwa walienda
makaburini tayari kwa mazishi.
Alisema kwenye eneo hilo la makaburi kuna mti mkubwa na ni mrefu ambao ulikuwa na Nyuki kwa muda mrefu wakati Naibu Askofu wa kanisa Katoliki Jimbo kuu la songea Padri Camillius Haule anaendelea na ibada ya Misa ya Mazishi Nyuki walianza kuwangata watu lakini ibada ya mazishi ilivurugika na watu wote kutawanyika
Alifafanua kuwa watu waliokuwepo kwenye eneo hilo walikimbia na kutokomea kusiko julikana lakini bahati mbaya Amaliya alishindwa kukimbia kwasababu alikuwa hana uwezo wa kutembea na nyuki walimshambulia na baadaye aliokolewa na kukukimbiza kwenye zahati ya kijiji cha Liula ambako baada ya kupokelewa alithibitishwa kuwa amekufa
Kamanda Mwombeji alieleza kuwa baadaye wananchi walitumia njia mbadala kwa lengo la kuwasambaratisha nyuki kwa kuwasha moto kwenye maeneo hayo kisha nyuki walitawanyika na kutokomea kusiko julikana na mazishi ya marehemu Komba yaliendelea majira ya saa 12 jioni
Alifafanua zaidi kuwa Amaliya mbawala amezikwa februari 14 mwaka huu majira ya saa 7 mchana kandokando ya kaburi la mtoto wake na misa ya mazishi inadaiwa kuwa iliendeshwa na
Naibu Askofu wa kanisa kuu Jimbo la Songea Padri Haule na Kuhudhuliwa na watu wachache huku wakiwa kimya kwa kuhofia kuvamiwa tena na nyuki hao ambao hawakuwepo eneo la tukio
MWISHO
Alieleza kuwa komba baada ya kufariki dunia jitihada zilifanywa za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka Liwale hadi kijijini Liula nje kidogo ya Manispaa ya Songea ambako walifika majira ya usiku wa kuamkia Jumamosi ya februari 13 mwaka huu.
Alisema kuwa baada ya kuufikisha mwili wa marehemu kijijini hapo taratibu za mazishi ziliendelea ambapo majira ya 9:30 alasiri wananchi wa kitongoji hicho wakiwemo wafiwa walienda
makaburini tayari kwa mazishi.
Alisema kwenye eneo hilo la makaburi kuna mti mkubwa na ni mrefu ambao ulikuwa na Nyuki kwa muda mrefu wakati Naibu Askofu wa kanisa Katoliki Jimbo kuu la songea Padri Camillius Haule anaendelea na ibada ya Misa ya Mazishi Nyuki walianza kuwangata watu lakini ibada ya mazishi ilivurugika na watu wote kutawanyika
Alifafanua kuwa watu waliokuwepo kwenye eneo hilo walikimbia na kutokomea kusiko julikana lakini bahati mbaya Amaliya alishindwa kukimbia kwasababu alikuwa hana uwezo wa kutembea na nyuki walimshambulia na baadaye aliokolewa na kukukimbiza kwenye zahati ya kijiji cha Liula ambako baada ya kupokelewa alithibitishwa kuwa amekufa
Kamanda Mwombeji alieleza kuwa baadaye wananchi walitumia njia mbadala kwa lengo la kuwasambaratisha nyuki kwa kuwasha moto kwenye maeneo hayo kisha nyuki walitawanyika na kutokomea kusiko julikana na mazishi ya marehemu Komba yaliendelea majira ya saa 12 jioni
Alifafanua zaidi kuwa Amaliya mbawala amezikwa februari 14 mwaka huu majira ya saa 7 mchana kandokando ya kaburi la mtoto wake na misa ya mazishi inadaiwa kuwa iliendeshwa na
Naibu Askofu wa kanisa kuu Jimbo la Songea Padri Haule na Kuhudhuliwa na watu wachache huku wakiwa kimya kwa kuhofia kuvamiwa tena na nyuki hao ambao hawakuwepo eneo la tukio
MWISHO
Chapisha Maoni