Kwirinus Mapunda- Songea.
MKURUGENZI wa Hospitali ya Peramiho Dr. Ansgar Stuff
(OSB) mewataka vijana kuinua vipaji vyao katika michezo ili taifa liweze kupata
wanamichezo bora kama nchi nyingine zilizoendelea
Hayo aliyasema mratiba wa
mashindano Sixbert Komba kwa niaba ya Dr Asgar Stuff ambaye anafadhili michezo
ya pasaka maarufu kwa jina la mashindano ya pasaka yanayofanyika Peramiho
Songea vijijini
Komba alisema michezo hiyo ya mpira wa miguu na pete yanajumuisha kata sita,
Maposeni peramiho Liganga, Mpandangindo, Litisha, Kilagano, Parangu madhumuni
ya mashindano hayo ni kuinua vipaji vya
wanamichezo wa mpira wa miguu na pete (netball).
Aidha mratibu huyo wa michezo hiyo Sixbert Komba
alisema mashindano hayo pia yana lengo la kuwaunganisha vijana kimwili na
kiroho na kuondokana na fikra potofu zenye madhara kimaisha na kuongeza kipato
kwa wananchi kwa kutoa fursa ya kufanyika biashara ndogondogo
Aidha alisema
mfadhili wa mashindano hayo atatoa zawadi kwa mshindi wa kwanza laki tano na
mshindi wa pili laki nne pia mshindi wa tatu laki tatu na mchezaji bora Tsh
Hamsini elfu katika ufunguzi wa michezo hiyo inayofanyika katika uwanja wa
Asgar Peramiho Songea vijijini
Alisema kuwa katika ufunguzi Parangu ilimenyana na Mpandangindo, matokeo
Parangu walichabangwa mabao 2 kwa sifuri, wafungaji ni Samuel Luambano Dk, 56
na Kandidus Lugongo Dk, 83
Alisema kuwa waamuzi walikuwa Kabanga Tambwe waamuzi wasaidizi
Kananani Kasuga na Hamisi Mapunda, aidha mgeni rasmi alikuwa Tanu Kameka kaimu
mkurugenzi wa Halmashauri ya Songea. Mashindano yanaendelea kila jumamosi na
jumapili
MWISHO
Chapisha Maoni